Pages

Wednesday, March 11, 2015

BREKING NEWS : Taarifa ya ajali ya basi la abiria iliyotokea Iringa leo…


Taarifa ambayo kwanza ilianza kuenea kwenye mitandao ya kijamii kuhusu ajali ya basi la abiria na lori la mizigo, kipindi cha Leo Tena Clouds FM wameongea na mashuhuda kutoka eneo la Changarawe, Iringa ambapo wamesema ni kweli ajali hiyo imetokea na kuna idadi kubwa ya watu ambao wamefariki.

Mashuhuda wamesema basi la Majinja lilitokea Mbeya kuja Dar es Salaam limegongana na lori la mizigo katika eneo hilo, abiria waliofariki ni wengi japo idadi kamili haijafahamika.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, kwa sasa yuko njiani kuelekea eneo la tukio ili kuona mazingira ya ajali na kutoa taarifa kamili kuhusu ajali hiyo.

CHANZO MILLARD AYO

No comments:

Post a Comment

TOA MAONI YAKO HAPA