Obama atadhibiti vipi udukuzi?


Rais Barack Obama
Rais Barrack Obama anajiandaa kutangaza ambavyo atarudisha imani katika idara ya ujasusi nchini humo kufuatia kufichuliwa kwa taarifa za idara hiyo na aliyekuwa mchambuzi wa maswala ya kijasusi nchini humo Edward Snowden.
Ufichuzi wa hivi karibuni uliochapishwa siku ya alhamisi unadai kuwa idara hiyo ya ujasusi ilidukua mamilioni ya ujumbe katika simu za watu za mkononi duniani kila siku.

Upelelezi huo wa simu zilizopigwa pamoja na mitandao umezua hisia kali kutoka kwa wanaharakati na makundi ya kijamii nchini marekani na washirika wake.

Hata hivyo vitengo vya ujasusi vimeonya kuwa uchunguzi zaidi wa mienendo yake huenda ukaathiri usalama wa marekani.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company