JE ,WAJUWA ? UTAMADUNI WA HII JAMII NI KUKATA VIDOLE WAFIWA

Utamaduni wa watu duniani unatofautiana, moja ya story ambazo sikuwahi kufahamu ni juu ya huu utamaduni wa jamii ya watu wa Dani iliyoko Magharibi mwa Papua, New Guinea ambapo utamaduni wao unahusisha inapotoke msiba wa ndugu yoyote basi ndugu wa marehemu wanaomboleza kwa kujikata vidole.

Hii imeshtua wengi walioisikia, kwa wale waliobahatika kuitembelea basi ni mashuhuda kwamba watu wengi wa kutoka jamii hiyo wamekatwa vidole na ndugu yoyote wa marehemu anakatwa vidole, umri sio kitu kinachoangaliwa sana hivyo hata watoto pia wanaguswa na hii moja kwa moja.

Utaratibu huo huwa unakuwa na ibada ya utangulizi ili kufukuza mapepo ya marehemu halafu linafuatia zoezi la kukata vidole, kwa utamaduni huo maumivu ya mwili huonyesha huzuni ya kufiwa pamoja na kuonyesha upendo kwa marehemu.

Hapa vidole vinakatwa kwa shoka, vipande vilivyokatwa vinachomwa moto halafu majivu yanahifadhiwa au kuzikwa pamoja na mwili wa marehemu.

Jitihada zimeanza kufanywa ili kuzuia utamaduni huo ambao madhara yake yameanza kuonekana kwa sasa

Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company