HABARI KUU ZA LEO na OSCAR SAMBA
print this page
HABARI NA Oscar Samba

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

Mahali: TAG Ushiri Rombo: Tarehe 28:2:2019. Na Mwalimu Oscar Samba.
.

Mwanzo 2:18 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.
Mwanamke ni msaidizi, andiko hilo lipo kabla ya dhambi kuingia ulimwenguni, hakukuwa na mfumo wa kanisa ama kuabudu kama leo, au kama baada ya dhambi, kusudio la ndoa, au familia ni ili liwe kanisa, yaani tuliumbwa kwa ajili ya ibada !

Kwa hiyo, kanisa, lina mukutadha wa ndoa, kwa hiyo, dhima ya mwanamke kindoa au kifamilia, ina mashabihiano na ile ya kikanisa !

Waefeso 5:23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili.
24 Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.

Kama ndivyo, mwanamke ameumbiwa kulichukulia kanisa kama anavyomchukulia mumewe, utendaji wa usaidizi kwa mume, ama kumuheshimu, uwe vivyo hivyo kwa kanisa, maana Kristo u kichwa huku.
Kumbuka hili Daima: Kuwa ni yule amchaye Mungu ndie asifiwaye: Mithali 31:30 Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa.

Jambo hili, likupe kuhakikisha una sifa ya uchaji, kama kweli unadhamiria kusifiwa na Kristo ambaye ndie kanisa, na hakika ukijipatia kibali au sifa njema kutoka kwa Bwana Yesu, ni umejipatia kutoka kwa kila mtu, jifunze kwa wakina Debora,Dorkasi, na wengine akiwemo yule Mariamu aliyempaka yale mafuta, hadi leo tukio hilo lingali likikumbukwa, sasa utafahamu kuwa utendaji wao mwema uliotokana na uchaji ndio uliopeleke kujizolea sifa hizo.

Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili ! Kwa hiyo ni hatari mno kujisifia vya mwilini, ila sifa zitokane na uchaji, ambao huzaa kazi njema !
MAJUKUMU YAKE KATIKA NAFASI KWENYE KANISA:

1.  Ni Mueneza Habari Njema, sifa njema kuhusu Mchungaji wake, kanisa lake, huduma ya kanisani, watumishi wa kanisani, na kila wasifu mzuri kulihusu.

Ni jukumu lake pia kumuelezea Kristo Yesu kwa wasio mjua, huyu ni mjumbe mzuri sana, maana mwanamke amepewa kinywa chenye uwezo wa kuzalisha maneno mengi, adui amekuwa akiwahi hili na kulitumia vibaya kwa umbea na misuto, ukizingatia pia amepewa uwezo wa kutoka mji huu ama nyumba hii na kwenda kwa ile, nia ni ili aeneze mema, ila adui amewatumia vibaya.

Mfano wa dhima hii kibiblia ni mwanamke yuke wa kisima cha Yakobo Msamaria: ( Yoh 4:7-42.) 

Alipofahamu uzuri wa Yesu, moja kwa moja aliacha mtungi wake na kwenda kueneza wema wake!

Yohana 4:28 Basi yule mwanamke akauacha mtungi wake, akaenda zake mjini, akawaambia watu.

Kuna wakina mama au mabinti unakuta anafua nguo,au kukatakata kitunguu jikoni, ghafula huepua sufuria na kwenda mbio kwa jirani baada ya kusia umbea fulani, huku ni kukosa kujitambua ! Akisikia neno mbio ataaga na kutoka kanisani mapema utazani anawahi mtoto nyumbani, kumbe kuna sumu anaenda kumwaga kwa mpendwa ambaye hajaja kanisani. 

Huyu Msamaria, kaacha mtungi, na kwenda kueneza habari za Yesu, wewe je unaacha na kwenda kueneza nini? Aibu ya kanisa, udhaifu wa mama mchungaji wako, udhaifu wa kiongozi wako wa idara, ama unapeleka madhaifu ya kikanisa kwa wapendwa na mbaya zaidi hata kwa wasio wapendwa yaani kwa watu wa mataifa ! Ila huyu, hakufanya hivyo!

Nisikilize, hakuna mtumishi aliyekamilika, wapo mbinguni, hakuna kanisa lililokamilika, hoja ni pale unapoona madhaifu unafanya nini? Unapaswa kuomba, ukiona doa kwenye koti langu, kachukuwe sabuni na maji uliondowe, sio kulipiga picha na kusambaza doa langu, hujanisaidia, na ukitangaza aibu ya mtumishi ni umeanika aibu ya Yesu, huko ni kulivua nguo kanisa, na kanisa ni Kristo, uwe na uhakika adhabu inakuhusu siku ile ya mwisho ! Jifunze sana kwa huyu mwanamke, nawe uwe ni mueneza habari njema kwa majirani zako, marafiki, usikubali kukaa nao na kujadili yasiyofaa, bali mjadili mema, mkiongea kumi kuhusu VIKOBA, na VIBATI, au mchezo wa fedha,basi wewe weka hapo mawili ya Yesu, anza tu stori kuwa nilipokuwa sijaokoka jamani nilikuwa na sumbuliwa na hili au lile, ila toka nimeokoka, naona nimepokea mujiza, usishangae jirani yako akikwambia, jamani nipelekeni na mimi hapo !

Ama, mchungaji wetu akikuombea, Mungu aliyeko ndani yake atakufungua haraka sana, hapo unafahamu kuna mgonjwa, hata kama hatatoa jibu muda huo uwe na hakika kuwa punde, au baada ya muda, Kuna siku atakutafuta tu, maana ulipanda mbegu, maneno ni mbegu !
(Mithali 6:19 Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.)

Sasa ikupe kujiuliza sana, huwa unapanda mbegu ipi uwapo kanisani, au na wapendwa, kama unamsema vibaya mchungaji, au kanisa, ama mpendwa, uwe na hakika, unapanda pando baya, na apandaye magugu ni mwana wa Ibilisi !

Tuendelee na utendaji wa mwanamke huyu, aliyemtengenezea Yesu mazingira mazuri ya kuifanya kazi yake !

Yohana 4:29 Njoni, mtazame mtu aliyeniambia mambo yote niliyoyatenda. Je! Haimkini huyu kuwa ndiye Kristo?
Na wewe tafuta ulilotendewa na Yesu, lipo, ( Kila aliye na Mwana hakosi ushuhuda, kama huna, tazama vyema kiroho chako kama kweli unaye Mwana !)

30 Basi wakatoka mjini, wakamwendea.
39 Na katika mji ule Wasamaria wengi walimwamini kwa sababu ya neno la yule mwanamke, aliyeshuhudia kwamba, Aliniambia mambo yote niliyoyatenda.

40 Basi wale Wasamaria walipomwendea, walimsihi akae kwao; naye akakaa huko siku mbili.
:41 Watu wengi zaidi wakaamini kwa sababu ya neno lake.
42 Wakamwambia yule mwanamke, Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu; maana sisi tumesikia wenyewe, tena twajua ya kuwa hakika huyu ndiye Mwokozi wa ulimwengu.

Yesu alikuwa na kazi nyepesi sana huku, hakukuwa na haja ya kulipia matangazo ya mkutano, au kusambaza vipeperushi, maana kuna mtangazaji, na msemaji wake, alimtangulia, nawe una hiyo dhima, hakikisha unatumia vyema nafasi hii!

Kumbuka hili siku zote, kuwa Mungu asiponufaika na alichoweka ndani yako, basi adui atakitumia, huamini, acha kumsema Yesu, usipojikuta unawasema watu ! Kanisani utakuwa mkosoaji na kuchambua mabaya kana kwamba hakuna jema hata moja, kiongozi wa migomo baridi ni wewe, mbeba maneno utakuwa ni wewe, kwa nini, chai iliyopoa au supu, ndipo nzi hutua ! Kama kinywani mwako Yesu habebwi, Ibilisi atabebwa, utashangaa kila baada ya maneno yako unasema lakini tumuombee, lakini kiukweli huwa hauombi ! 

2. Ni Muombaji; Yohana 2:3 Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai.
4 Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia.
:5 Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni.

Sijajua ni kwa nini, ila wanawake wamepewa nafasi ya maombi yao kuwa na wepesi na kibali cha haraka sana, labla kwa kuwa ndani yao uombolezaji ni mwepesi zaidi, ila ninachonuia kukwambia hapa ni kwamba uonapo tatizo au upungugufu kanisani, sio muda wa vikao, na kuchambua, bali ni muda wa kufanya maombi, au dua, ama toba, lishike hili siku zote !

3. Ni Chanzo cha Utatuzi wa Migogoro au Matatizo Sugu maana amepewa Busara na Hekima; Mfano 1, Abigaeli; ( 1 Samweli 25:4-35.)
1 Samweli 25:23 Ndipo hapo Abigaili alipomwona Daudi, alifanya haraka kushuka juu ya punda wake, akamwangukia Daudi kifulifuli, akainama mpaka nchi.

24 Akamwangukia miguuni pake, akasema, Juu yangu, bwana wangu, juu yangu mimi na uwe uovu; tafadhali mjakazi wako na anene masikioni mwako, nawe uyasikilize maneno ya mjakazi wako.

25 Nakusihi, bwana wangu, wewe usimwangalie huyu mtu asiyefaa, yaani, Nabali; kwa maana kama lilivyo jina lake ndivyo alivyo yeye; jina lake ndilo Nabali, na upumbavu anao; lakini mimi, mjakazi wako, sikuwaona hao vijana wa bwana wangu aliowatuma.

32 Naye Daudi akamwambia Abigaili, Na ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye amekuleta hivi leo kunilaki;

33 na ibarikiwe busara yako, na ubarikiwe wewe, uliyenizuia hivi leo nisimwage damu, wala kujilipiza kisasi kwa mkono wangu mwenyewe.
Mfano 2, Kisa cha Seba aliyemuasi mfalme Daudi ! 

Baada ya tukio hili, Yoabu alinuia kuleta maangamizi makubwa kwa mji wao wote, na tayari alishaanza kuuvunja ukuta, nasi twafahamu huluka ya Yoabu, katika hiyo sura tu alikuwa ametoka kumuangamiza mtu kwa kukita upanga tumboni mwake, Abineli aliuawa naye, japo alikuwa ameshatengeneza, pia Absolum aliuawa, japo mfalme aliachilia rai ya kumtaka aishi ! Kwa hiyo, sio ajabu kuwa mji huo,ungedhuriwa !

Ila kwa hekima ya huyu mwanamke atwajaye kama mwenye akili, huku biblia nyingine za kingereza na zile za kiswahili rahisi kutumia neno mwenye busara,aliweza kuuokoa mji huo, sasa kanisa likiwa na mama mchungaji makini, na mumewe kujua kumtumia vyema, kwa kumsikiliza na kumpa nafasi, uwe na uhakika atafanikiwa kupindua maamuzi ambayo yangeweza kuleta madhara kwa kanisa, kama Abigaili na huyu waliweza, ni fika hata wewe wa weza !

Kuna ina fulani ya hekima, na busara, na uwezo wa ushawishi waliopewa wanawake, sasa adui akiuwahi, hapo huzalisha wakina Delila,ila Kristo kiuwahi, huzalisha wakina Abigaili, sijui wewe u wapi, au umempa nafasi adui au Kristo Yesu ! 
Tuuone mfano wetu : 

2 Samweli 20:15 Na hao wakaja wakamhusuru katika Abeli wa Bethmaaka, wakafanya chuguu mbele ya mji, nayo ikasimama kuielekea ngome; na watu wote waliokuwa pamoja na Yoabu wakavunja-vunja ukuta, wapate kuubomoa.

:16 Ndipo akalia mwanamke mmoja mwenye akili toka mjini, Sikieni, sikieni; mwambieni na Yoabu, aje hapa karibu, niseme naye.
:17 Basi akamkaribia; na yule mwanamke akasema, Ndiwe Yoabu? Akajibu, Ndimi. Ndipo akamwambia Sikia maneno ya mjakazi wako. Akajibu, Mimi nasikia.

18 Kisha akanena, akisema, Watu hunena zamani za kale, wakisema, Wasikose kuuliza huko Abeli; ndivyo walivyomaliza shauri.
:19 Mimi ni wa hao wenye amani, walio waaminifu katika Israeli; wewe unatafuta kuuharibu mji, na mama wa Israeli; mbona wataka kuumeza urithi wa Bwana?

:20 Yoabu akajibu, akasema, Isiwe, isiwe kwangu, niumeze wala kuuharibu.
21 Neno hili silo hivyo; lakini mtu mmoja wa milima ya Efraimu, Sheba, mwana wa Bikri, jina lake, ameinua mkono wake juu ya mfalme, naam, Daudi, basi mtoeni yeye tu, nami nitaondoka katika mji huu. Basi yule mwanamke akamwambia Yoabu, Tazama, kichwa chake utatupiwa juu ya ukuta.

:22 Ndipo yule mwanamke akawaendea watu wote katika akili zake. Nao wakamkata kichwa Sheba, mwana wa Bikri, wakamtupia Yoabu huko nje. Ndipo akapiga tarumbeta, nao wakatawanyika kutoka mjini kila mtu hemani kwake. Naye Yoabu akarudi mpaka Yerusalemu kwa mfalme.

Mwanamke ! Mumeo akiwa mkali, akiwa na hasira kama simba, ni hatari wewe ukiwa kama mbuzi, ila ukiwa kama kondoo, utafanikiwa kuituliza, huyu mwanamke kama naye angeinuka na kujibizana, hakika angechochea ghadhabu ya Yoabu, ila alitumia busara, sasa wanawake wengine, nao hupanda juu, hawajui Mithali 15:1 husemaje ? Kuwa jibu la upole hutuliza hasira, ila la kinyume chake huchochea !
Biblia nyingi za kingereza zimetumia neno ulimi laini, au mzuri, kwa hiyo, ukitaka kutenda vyema, dhidi ya mumeo mwenye hulika kama ya Yoabu, hakikisha unakuwa na ulimi laini, maana hata vyuma bila mafuta husagika.

Akikuudhi na wewe ukisema naenda kwetu, usishangae akiwa wa kwanza kukutolea begi nje!

Sio kwamba hakupendi, ila umechochea ghadhabu, ndio maana ukiondoka, baada ya siku mbili tatu, anakufuata, hapo uwe na hakika, hasira imeisha ! Sasa unaweza kuituliza kwa akili, sio kwa kushindana, huyu mwanamke na Abigaili wawe ni somo tosha kwako !

Muone Ambaye anatumiwa na Ibilisi, ni Mvunjaji, ni mbomoaji, nyundo, huweza kujenga ikitumiwa katika dhamira hiyo, ila ikitumiwa vibaya hubomoa pia, kwa hiyo chombo hakina shida, mtumiaji ndie mwenyewe shida: Kwa hiyo kama kuna mwanaume anaoma huu ujumbe, ajuwe sasa kumuombea mwenzie ! Na kama ni mtumishi, ukiwa na wanawake waharibifu, jifunze kuwabadili au kubadili nia zao kupitia maombi na mafundisho !

Mithali 14:1 Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.

Ona hapa: 

Mithali 27:15 Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi, Na mwanamke mgomvi ni sawasawa;

Oanisha na : Mithali 19:13 Mwana mpumbavu ni msiba kwa babaye; Na ugomvi wa mke kama kutona-tona daima.

4. Hutunza Watumishi; 1. Yule Mshunami; 2 Wafalme 4:9 Yule mwanamke akamwambia mumewe, Tazama, mimi naona ya kuwa mtu huyu apitaye kwetu mara kwa mara ni mtu mtakatifu wa Mungu.

10 Nakuomba, tumfanyie chumba kidogo ukutani; na ndani yake tumwekee kitanda, na meza, na kiti, na kinara cha taa; na itakuwa, atujiapo, ataingia humo.

Kuna mzigo wa kipekee ambao Mungu ameweka kwa wanawake kuhusu kuwahudumia watumishi, na kanisa lenye wanawake wenye kujitambua kama hawa, moja kwa moja, hutimiza dhima hii vyema sana !

Mfano 2, Mwanamke wa Serepta, 1 Wafalme 17: 10-16. 

Mfano 3, Enzi za Yesu, japo hata kwa Paulo Mtume ama kqnisa la kwanza walikweo wakina Lidia, tumuone Yesu; 

Luka 8:2 na wanawake kadha wa kadha ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba,

3 na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao.

Yesu alihudumiwa kwa mali zao, wewe jiulize, mtumishi wako unamuhudumia kwa mali zako ! Na Yesu wa leo ni huyo mlawi wako, ama mtumishi wake !

Na kama hujaokoka na unataka kufanya hivyo sasa tafadhli kwa imani kubwa nakuu kabisa fuatisha pamoja nami maneno haya, au sala hii ya toba ili uweze kuokoka, Sema;

BWANA YESU, NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NATUBU MBELE ZAKO LEO, NISAMEHE NA NINAKUOMBA UFUTE JINA LANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU, TAFADHALI LIANDDIKE KWENYE KITABU CHA UZIMA, NINAKUKIRII NA KUKUPOKEA MOYONI MWANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, HAKIKA WEWE NI MUNGU NA ULIFUFUKA KATIKA WAFU, Amen.

Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo, kwa maombi, sadaka kwa njia ya M-Pesa, kupiga simu au Wasats App, ni +25559859287. Tupo Arusha Tanzania.
0 Toa maoni yako.

MAANA YA MBEGU ILIYODONDOKA KANDO YA NJIA

HABARI ZETU
Mahali: TAG Ushiri, Rombo:     Tarehe 27/2/2019, Na Mwalimu Oscar Samba

Mathayo 13:3 Akawaambia mambo mengi kwa mifano, akisema, Tazama, mpanzi alitoka kwenda kupanda.
4 Hata alipokuwa akipanda, mbegu nyingine zilianguka karibu na njia, ndege wakaja wakazila;
( Luka, zikakanyagwa:Luka 8:5 Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake; naye alipokuwa akizipanda, nyingine zilianguka karibu na njia, zikakanyagwa, ndege wa angani wakazila.)
19 Kila mtu alisikiapo neno la ufalme asielewe nalo, huja yule mwovu, akalinyakua lililopandwa moyoni mwake. Huyo ndiye aliyepandwa karibu na njia.
Kwa hiyo, kutokulielewa neno, huifanya mbegu hiyo kukosa makao mazuri moyoni mwa muhusika, maana hapo huambiwa yule asikiaye, lakini asielewe yu sawa ama ndie aliyepandwa kando au pembezoni mwa njia, ambapo adui huja na kulitwaa hilo neno, ama kukanyagwa na kuharibiwa.
Maana ya Mbegu: Mbegu ni Neno la Mungu, mpanzi ni Muhubiri, ama Roho Mtakatifu moja kwa moja, au kumpitia mjumbe wake aliye Mtumishi wake;
Luka 8:11 Na huo mfano, maana yake ni hii; Mbegu ni neno la Mungu.
Shamba ni Moyo: Luka 8:12 Wale wa karibu na njia ndio wasikiao, kisha huja Ibilisi akaliondoa hilo neno mioyoni mwao, wasije wakaamini na kuokoka.
Kama huondolewa moyoni, maana yake lilipandwa hapo, kwa hiyo, kama mbegu ni neno, na moyo ni shamba, kwa mantiki hiyo mahubiri, au mafundisho hupandwa moyoni mwa muhusika.
Zile aina za mahali mbegu zilidondokea, yaani njiani, penye udongo mchache, penye miiba, na udongo mzuri, maana yake ni aina ya mioyo ya watu wanaolisikia neno la Mungu.
Mpanzi au mkulima apandapo, ili mbegu iwe imedondokea sehemu ipi, ni matokeo ya moyo ulio nao, kwa hiyo ukitaka kuwa na mafanikio, ni lazima kuhakikisha unajitengenezea moyo mzuri, ili neno lijapo, lidondoke mahali sahihi.
Kusudi la Mungu Kukutaka Mbegu yake Isipandwe kando ya Njia.
Kumbuka sana kuwa Mungu kama mkulima hataki au hapendi kupanda njiani, ila mazingira ya moyo wako ndio huifanya mbegu kuelekea hapo !
1. Ili Kuua na Kuuhuisha; Yohana 12:24 Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi.
25 Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa mikulala
26 Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.
Kitu neno hufanya ni kuua aina fulani ya maisha yasiyo ya Kiungu, na kuhuisha yaliyo sahihi, Warumi hutuambia vyema kuwa kufa kwa Yesu ni kuua mwili wa dhambi na kufufuka ndimo mlimo na mantiki ya kufufua utu mpya.
Mungu akitaka kuua visivyo vya kwake kwako, na kuhitaji kuhuisha vya kwake, huliachilia neno lake, au mbegu yake, sasa ikianguka mahali sahihi, ndipo hufanikiwa sana, unaposikia alikuwa mwizi na kuacha, maana yake, alipokea neno lililouwa wizi na kuhuisha uadilifu,ambao ni tunda la Kristo.
2. Kukufanya Uzae, na Huwezi zaa kama mazingira sio rafiki kwa uzalishaji, mfano wa mazingira rafiki;
Mathayo 13:23 Naye aliyepandwa penye udongo mzuri, huyo ndiye alisikiaye lile neno, na kuelewa nalo; yeye ndiye azaaye matunda, huyu mia, na huyu sitini, na huyu thelathinhuu.
Kwa hiyo, ukihitaji kuwa na utumishi wenye mafanikio kwako, kuhakikisha kuwa unajiwekea mazingiira mazuri ya kupokea neno la Mungu linalonuia kukubadilisha kitumishi ni muhimu sana, ukihitaji kufanikiwa kimaisha, ni shariti moyo wako uwe na mazingira rafiki katika uzalishaji wa matunda na  hauwezi zaa, kama mbegu haijamea, ikidondoka njiani, haitamea, ya udongo haba au juu ya mwamba, itanyauka yakija mpito, na ile iliyosongwa haiwezi kuivisha kama Luka isemavyo.
Ujumbe huu ni jibu tosha na muhimu sana kwa yule anayehitaji kufanikiwa, au kustawi kihuduma, kimaisha, na kuwa mti mkubwa kama ufalme wa mbinguni ufafanuliwavyo, wengi hutamani sana kufanikiwa kihuduma, ila kuna mahali wamekwama, ambapo ni hapa, mfano utakaouona hapo mbeleni wa mti ulioanza na mbegu ndogo na kisha kupanuka na kuzaa,na ndege kukaa juu yake, ni muhimu kujua kuwa, asili yake ni mbegu, ila sio iliyodondoka njini, wala kusongwa, wala juu ya mwamba, bali ni ile ya udongo au moyo mzuri, kwa hiyo, nawe ukihitaji kufanikiwa katika jambo fulani ni lazima kujua au kuijua hii Kanuni !
Nakupa tena maandiko kuhusu dhima ya mbegu, katika kuuwa na kuhuisha kitu fulani, maandiko haya yakupe kuhakikisha unanufaika vilivyo na neno la Mungu, kama kuna vitu ndani yako huvitaki, na untaka vichipuke vya kiungu, maandiko haya hunena habari za nyakati za mwisho kuhusu kubadilishwa kwetu, ila hapa nataka ujionee thana ya mbegu, na ili iwe na matunda lazima ife, kufa ni kubadilika, kutoka katika mbegu, na kutoa mche, neno la Mungu lililopo kwenye biblia halina matunda hadi liingie moyoni mwako, na kuanza kuzalisha mabadiliko! Mbegu ambayo haijafa,ni mbegu, sasa hatutaki mbegu, tunataka matunda, na ili tuyapate ni lazima tupande, kisha imee, sasa wengi kiroho hutaka mbegu, ila kubadilishwa au kuiruhusu, ama kuipa nafasi ili iwabadilishe, kisha wawe na matunda hawataki, atakuwa ni mkulima wa ajabu sana ambaye ataishilia kununua mbegu, ila hataki mazao ! Na ndivyo wakristo wengi walivyo leo, husoma sana neno, huenda sana kanisani, ila hawairuhusu injili iwabadilishe! Usizini, usiibe, wahi kanisani, uwe mtoaji, toa zaka kamili, ila bado wako pale pale, hawaruhusu neno hilo, kuingiza mabadiliko mapya ndani yao, tujionee maandiko !
(1 Wakorintho 15:35 Lakini labda mtu atasema, Wafufuliwaje wafu? Nao huja kwa mwili gani?
36 Ewe mpumbavu! Uipandayo haihuiki, isipokufa;
:37 nayo uipandayo, huupandi mwili ule utakaokuwa, ila chembe tupu, ikiwa ni ya ngano au nyingineyo;
:38 lakini Mungu huipa mwili kama apendavyo, na kila mbegu mwili wake. )
Kumbuka/ Fahamu: Mungu ni Mpanzi, na Shetani naye ni Mpaanzi, kwa hiyo moyo wako usipopandwa mbegu njema, utapandwa mbaya, na nia ya mbegu njema, ni Ufalme wa Milele;
(1 Petro 1:23 Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele. )
Mungu alipoiumba dunia, alipanda pando jema, adui akaja, baada ya kulala kwa Adamu, akapanda pando baya, hii ikupe kuenenda kwa umakini humu ulimwenguni;
Mathayo 13:24 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;
:25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
:26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.
27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?
Ukindelea mbele ya hayo maandiko utapata kujua kuwa magugu yanatakiwa kuachwa hadi siku ya mavuno, kwa hiyo inawezekana nawe katika kwaya, au utumishi ama kanisani u gugu, ila bado umeachwa haimaaniishi parapanda ikilia nawe utakuwa mawinguni, la!
Bali utaingia jehanum ya moto, hekima ya kuachwa kwa magugu haikupi kuingi mbinguni, maana siku ya mavuno, itachambuliwa ngano na kufungwa matitamatita, kisha kuwekwa ghalani, na magugu nayo yatafungwa, ila yatatupwa motoni, na huko ndimo mlimo kilio na kusaga meno, sasa hii ikupe kutengeneza na Bwana, yaani uruhusu mbegu njema, ambapo mimi kama mpanzi kwa uweza wa Mpanzi Mkuu, ninanuia kupanda moyoni mwako leo, au majira haya, ili sasa pando jema liwe ndani yako, na kuuwa kila pando baya, yaani ufisadi, ulafi, uasherati, wizi, matukano, kiburi, dharau na kadhalika.
3. Kumbuka Hauwezi Kufika Hapa kama Mbegu yako haikupandwa Sehemu sahihi; Mathayo 13:31 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na punje ya haradali, aliyoitwaa mtu akaipanda katika shamba lake;
32 nayo ni ndogo kuliko mbegu zote; lakini ikiisha kumea, huwa kubwa kuliko mboga zote, ikawa mti, hata nyuni wa angani huja na kukaa katika matawi yake.
Ni dhairi kuwa ukihitaji kuinuliwa, au kupanuka kimaisha na kiroho, na kihuduma, ni lazima kuhakikisha kuwa moyo wako una mazingira sahihi katika kulipokea, na kulitunza neno la Mungu, mkulima makini huliandaa shamba vyema na kulitilia mbolea, nawe kama Mkristo makini, hakikisha moyo wako ni uliopondeka.
Isaya 66, hutuambia kuwa mtu ambaye akilisikia neno la Bwana hutetemeka, huyo ndiye Mungu humuangalia, kwa maana kwamba huyu mtu moyo wake, u na mazingira mazuri, akionywa huonyeka, akihaswa huzingatia, iwe hivyo kwako !
Madhara ya Kupandwa Kando ya Njia, au Nia ya Adui Anapoweka Mazingira moyoni mwa mtu ili Neno lipandwe kando ya Njia:
Kuna vijitabia ambavyo Shetani huvitumbukiza ndani ya moyo wa mtu, na wengi hawajui ni kwa nini ! Nia yake ni kumuwekea muhusika mazingira ya mbegu au neno alisikialo lisidondoke sehemu sahihi !
Mathalani kiburi, huyu mtu asikii maonyo, asikii mahusia, maana njia yake imenyooka machoni pake mwenyewe, ikiwa na maana kwamba kile akiwazacho, akionacho, akipangacho hukiona ni sahihi hata kama atashauriwa, kwenye kiburi kuna upumbvu, pia ujinga, ukija katika Obadia 1:3-4, utagundua kuwa kiburi pia hudanganya, yaani hupotosha, kwa hiyo kitamuaminisha kuwa njia hii ni sahihi, wazo hili ni sahihi, kama ilivyokuwa kwa mfalme Sauli, maana kiburi kilimpa kujiamini hata kama Mungu atakuwa amemuacha, maana kii na mbinu na tabia ya kudanganya, mtu hujiona yu salama kumbe sivyo !
Mazingira mbayo ni hatarishi sana kwa Neno kuweza kuchipusha linalotakiwa kuhipusha !
1. Ili Aweze Kuinyakuwa, au kuiharibu, ama Kuizuilia Isichipuke: Luka 8:12 Wale wa karibu na njia ndio wasikiao, kisha huja Ibilisi akaliondoa hilo neno mioyoni mwao, wasije wakaamini na kuokoka.
Unapohubiri na mtu kusema ananisema, au moyoni mwake kuwa na mawazo mengine, kimawazo kuwa mbali ama kiakili,ama anapofanikiwa kubana akili ama fikra zake, au ufahamu wake ili asielewe, uwe na uhakika kuwa baada ya mahubiri, au neno hilo, adui huja na kulinyakuwa, ama hukanyagwa !
2. Ananuia Kukuzuilia Kunufaika na Kile Kilichokusudiwa na Mpanzi; Yohana 12:40 Amewapofusha macho, Ameifanya mizito mioyo yao; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakafahamu kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya..
Wakati wakina Bartomayo kipofu wakipokea miujiza yao, Mafarisayo, haikuwa hivyo kwao, hakuna mahali wananufaika na injili yaa Yesu isipokuwa Nikodemu aliyejua kuweka kiburi cha kidini na elimu pembeni na kukubali kunyenyekea, sio kwamba hawakuwa na mahitaji la! Walikuwa nayo, ila tatizo ni mioyo yao kugoma kuipokea hiyo mbegu !
Sasa maandiko hayo hutuambia kuwa ni ili wasije wakapokea nuru ama mwanga kisha kuweza kuponywa na Kristo Yesu, kwa hiyo, unapohubiri na watu kutema chakula, maana yake, adui amefanikiwa kuwazuilia kubadilishwa na hilo neno, dalili kubwa ya mtu ambaye mbegu haijadondoka njiani ni mabadiliko yake, ukiwa na mshirika asiyebadilika, kuwa makini na shamba upandalo mbegu, kama hana kiburi, sio mwenye madharau, na mkataa maonyo, basi ombea ufahamu wake, maana kuna namna umefungwa,katika mpanzi huambiwa kuwa mtu anapolisikia hilo neno na kushindwa kulielewa hapo ndipo huja adui na kulinyakuwa, kwa hiyo adui akifanikiwa kuzuilia au kubana uekewa wako ama wake uwe na uhakika amezuilia jambo kubwa sana.
Katika kitabu chetu cha IJUWE HUDUMA YA UINJILISTI, nimewataka wainjilisti kuhakikisha kuwa wanaombea hii mioyo, yaani wanaandaa hili shamba vyema, ila katika upandaji, waweze kupanda mahali sahihi, hakuna mpanzi atakaye kupanda njiani, ama mahali pasipo mzalia matunda !
Sasa wachungaji, na wale wanaombea ibada, ni lazima sana kujifunza kuelewa usikiaji wao, fahamu zao, kama akikamata fikra, ama mioyo yao na kuitia uzito hufanikiwa kuwazuilia kupata wokovu, basi wewe ombea hizo fikra ziangushe hizo ngome za mawazo mbaya, na kila fikra zijiinuazo kinyume na elimu ya Kristo, kisha zitiishe, hii ni siri kubwa sana,hakikisha unaombea usikiaji wao, maana hapo ndipo adui huwekeza sana, ndiposa wakati wa ibada hujitahidi sana kupambana na usikiaji wao, asipoamisha mawazo, basi atafinya hata mtoto ili aliye, kwa nia ya kuondoa usikivu !
3.
Mazingira Rafiki na Hatarishi kwa Mbegu:
1. Roho na Tabia ya Kupuzia Maonyo, au Mahubiri, ama Mafundisho, ama Makaripio: Mithali 1:28 Ndipo watakaponiita, lakini sitaitika; Watanitafuta kwa bidii, wasinione.
29 Kwa kuwa walichukia maarifa, Wala hawakuchagua kumcha Bwana.
30 Hawakukubali mashauri yangu, Wakayadharau maonyo yangu yote.
31 Kwa hiyo watakula matunda ya njia yao, Watashiba mashauri yao wenyewe.
32 Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza.
33 Bali kila anisikilizaye atakaa salama, Naye atatulia bila kuogopa mabaya.
Kuna Hatari ya Kupotea, na hata Kufa: Mithali 5:23 Atakufa huyo kwa kukosa maonyo, Naye atapotea kwa wingi wa ujinga wake.
Suluhu lake: Tilia Moyoni, Luka 2:49 Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?
50 Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia.
:51 Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.
Mamaye na Yesu, hakuwa kama wengine, alitilia moyoni, hapo ukiniuliza sababu ya wengine kutokutilia moyoni, nitakwambia i katika huo mstari wa 50, kwamba hawakuelewa, sasa utaniele ni kwa nini adui huhakikisha kuwa watu wakisoma biblia hawaelewi, wakisikiliza mahubiri hawaelewi, huishilia kusema kile kitabu ni kizuri, somo alihubiri visuri, ila mulize alichoambulia hapo, hana! Anachokumbuka ! Labla kichekesho ama kitu kilichomfanya ama kuwafanya kucheka! Hii ni hatari sana.
Sasa ikupe kuhakikisha unapoonywa, unapokatazwa, unatilia moyoni unayoambiwa, unaposikiliza neno na kugundua dosari yako hapo, kinachotakiwa kufuata ni mabadiliko, ukisikia injili ya onyo kwa wasiotoa zaka,moja kwa moja anza kutubu, kisha msihi Mungu akuumbie tabia na mwenndo mpya, sasa huyu ndiye anayeitwa kuwa humfurahisha Mungu, ama ndiye mtu ambaye Mungu humtazama, tumuejionea kwenye Mithali hapo juu kuwa wapo wamuitao, ama wamtafutao kwa bidii ila hawamuoni, maana wamekataa maarifa, na sababu ni kudharau monyo, sasa leo tuna waombaji wazuri sana, wanataka kumuona Mungu kwenye jambo fulani, ila hawajui kuwa ameshagoma kuwasikiliza maana alinyoosha mkono hawakuutazama, wanamtafuta kwa bidii ila kauficha uso wake kwa maana walikwepa maonyo !
( Kutilia Moyoni ni Kuhifathi: Mwanzo 37:11 Ndugu zake wakamhusudu; bali baba yake akalihifadhi neno hili.)
Ona Mukutadha wa Kutokutilia Moyoni hapa: Isaya 42:18 Sikilizeni, enyi viziwi; tazameni, enyi vipofu, mpate kuona.
19 Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu? Au aliye kiziwi, kama mjumbe wangu nimtumaye? Ni nani aliye kipofu, kama yeye aliye na amani? Naam, kipofu kama mtumishi wa Bwana?
20 Unaona mambo mengi, lakini huyatii moyoni; masikio yake ya wazi, lakini hasikii.
Pili Kubali kuonywa; Kusudi la Maonyo ni Kukugeuza: Mithali 1:23 Geukeni kwa ajili ya maonyo yangu; Tazama, nitawamwagia roho yangu, Na kuwajulisheni maneno yangu.
24 Kwa kuwa nimeita, nanyi mkakataa; Nimeunyosha mkono wangu, asiangalie mtu;
:25 Bali mmebatilisha shauri langu, Wala hamkutaka maonyo yangu.
Nia na kusudio kubwa la maonyo ni kukugeuza, kama huo mstari wa 23 uanzavyo, ni sawa na mtu anayetaka kuelekea uwanja wa ndege wa KIA, ila kapanda gari la kuelekea Dar es salam, na kashafika Tanga, anaulizwa na mtu unaenda wapi, KIA, anaambiwa kuwa umepeotea, geuka,anagoma, sasa ni sawa na mtu anayeonywa, kuwa ukitaka kufanikiwa kielimu, achana na ngono, ukitaka kufaulu, acha kiburi, ila bado ni jeuri, baada ya muda, hujikuta amepotea, ila akisiliza, hugeuka, na hapo huelekea njia iliyo salama !
Kuna mahali maonyo hukuelekeza na kukuwezesha kufika, maana ni njia;
Mithali 6:23 Maana maagizo hayo ni taa, na sheria hiyo ni nuru, Na maonyo ya kumwadilisha mtu ni njia ya uzima.
Maonyo kuna kitu yamebeba, ukiyakubali, huweza kunufaika na kilichobebwa nayo, mfano hekima; Mithali 29:15 Fimbo na maonyo hutia hekima; Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.
Na kama hujaokoka na unataka kufanya hivyo sasa tafadhli kwa imani kubwa nakuu kabisa fuatisha pamoja nami maneno haya, au sala hii ya toba ili uweze kuokoka, Sema;

BWANA YESU, NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NATUBU MBELE ZAKO LEO, NISAMEHE NA NINAKUOMBA UFUTE JINA LANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU, TAFADHALI LIANDDIKE KWENYE KITABU CHA UZIMA, NINAKUKIRII NA KUKUPOKEA MOYONI MWANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, HAKIKA WEWE NI MUNGU NA ULIFUFUKA KATIKA WAFU, Amen.

Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo, kwa maombi, sadaka kwa njia ya M-Pesa, kupiga simu au Wasats App, ni +25559859287. Tupo Arusha Tanzania.

0 Toa maoni yako.

KITABU CHA WITO WA KITUMISHI. Na Mwalimu Oscar Samba wa Ug Ministry.

Ni Ujumbe uliopo kwenye hicho kitabu mada ya Mwisho inayoelekeza namna ya kuingia Shambani au kuanza huduma;

 Kumekuwa na tatizo kubwa sana kwa watumishi wengi wa leo, wanazitaka ishara na miujiza, pamoja na vitu vya mwilini kabla hawajaenda kuanza huduma.

Wanasahau maandiko husema kuwa ishara hizo zitaambatana na hao waaminio, ikiwa na maana kitu cha kwanza ni wao kuingia shambani, ndiposha ishara, na miujiza na mafanikio au vitendea kazi vya mwilini kama vyombo, majengo na hata mwanamke mjane wa sarepta hutokea kazini.

Siku moja wakati Roho ananifudisha jambo hili, alinipa mfano wa ajabu sana, aliniambia; Si unawaona madereva na magaria ya dalala, na makondakta wake, nami nilijibu ndiyo.

Ingekuwaje kama wangekaa nyumbani, au walipopaki magari yao, na kuanza kupiga debe wakiwa hapo, wangepata abiria?
Nalijibu hapana! Yenye alama ya mshangao, ndipo aliponiambia na watu wangu huwa katika mfano huo, wanapiga debe, ya kwamba gari lao linaelekea mahali fulani, lakini hawapo tayari kuliendesha na kuingia barabarani, yaani huanza kutafuta abiria, wakiwa au gari likiwa ndani, limeifadhiwa, bila kuliwasha na kuanza kazi barabarani.

Lakini madereva wa dunia hii, hulitoa gari lilipohifadhiwa wakiwa hawana abiria, ila wanapofika njiani au kituoni huanza kupiga debe na hatimaye kupata abiria, ikifika jioni, wana hesabu ya tajiri au ya gari, na wao wana riziki zao.

Watu wangu wasiowasha gari na kuanza kazi, nao ikifika jioni wanataka riziki zao, angali hawana hesabu ya tajiri, au ya gari.
Kwa hiyo hawana budi kuingia barabarani, maana huduma tayari nimeshawapa, ambayo ni gari. 

Mpendwa jambo hili ni kubwa, nalo ni pana, lina hitaji kulifahamu, maana ni kweli hata anayeuza duka, anapofungua asubui hajui atakayemuuzia, lakini wateja huja, na wewe huna budi kuanza huduma, wateja yaani washirika watakuja, na vitu kama vyombo, vya matangazo, na usafiri, vitakufuata tu.

Swali: Kuna abiria anayelipa nauli bila kuona gari? Sasa mbona wewe unataka vya mwilini bila kuingia shambani?
Kama Mungu akikujalia kukupa kabla, ni vyema, ila usimpangiye, ifanye kazi yake, kwa kutumia kipengele kile cha kuwa tayari kutumika popote, na ukumbuke Mwana wa Adamu hana pa kukilaza kichwa chake, ikiwa na maana ya kwamba, mazingira yoyote yasikuzuiliye kuifanya kazi ya Mungu.

Marko 16:17 Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya.
Biblia ya mafafnuzi, imetumia lugha nyepesi kidoko katika zitafutana;

(17Na ishara hizi zitaandamana na wale wanaoamini: kwa jina langu watatoa pepo na watasema
kwa lugha mpya.)

Ya Basic English imetumia neno ishara hizo zitakuwa nao hao wenye imani na jina langu;
(Mark 16:17 And these signs will be with those who have faith: in my name they will send out evil
spirits; and they will make use of new languages;)
Na ya King James Version, Imetumia neno, zitawafwata, maana yake, waende, alafu zije;

(17 And these signs shall follow them that believe; In my name shall they cast out devils; they shall speak with new tongues;)
Sasa chukua neno, Zita-wafwata, Zitakuwa nao, kuandana, na kufuatana, maana yake, ili kuvipata hivyo, unapaswa kwenda, navyo vije, usipofungua duka, na wateja wasipokuja, usilaumu wateja au muajiri wako, bali jilaumu wewe maana unapaswa kulifungua hilo duka, ndipo waone bidhaa, hakuna mtu ananunua mbuzi aliyepo kwenye gunia au kiroba, ni shariti aonekane kwanza.

Alafu pia hilo andiko linasema waaminio, au wanaoliamini jina la Yesu, nawe unapaswa kuwa na imani ya kwamba Yesu atakutokea tu, huko uendako, yupo kunguru atakayekutunza, wala usihofiye vya mwilini ya kwamba vitakuwaje.
Hakuna vyombo, hubiri bila vyombo, vitakuja tu, maana hata Yesu hakutembea na punda siku zote alizokuwa akiingia Yerusalemu, ila ipo siku aliingia na punda.

Sio kila mahali Yesu alihubiri juu ya jukwaa, ni mara chache sana alipata ofa za mitumbwi/boti na kuitumia kuingai ndani yake, na wakati mwingine alikuwa akikwepa makutano waliokuwa wakimsonga sana, pia na ili aweze kufikisha ujumbe vyema maana akiwa majini upepo wa mawimbi husafirisha sauti, nawe kuna siku utakutana na mtuimbwi wa wakina petro na kuupanda, yaani utapata jukwaa tu, wala usiwe na shaka.

KITABU KIKITOKA USIKIKOSE

Kama hujaokoka na unataka kuokoka ama ulirudi nyuma kiroho na unataka kutengeneza na BWANA kwa upya leo, tafadhali fwatisha nami maneno haya kwa Imani, Sema: BWANA YESU, NINAKUPENDA, NINAKIRI NA KUAMINI MOYONI MWANGU KUWA WEWE NI MUNGU, ULIKUFA NA KUFUFUKA KWA AJILI YANGU, INGIA NDANI YANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU LEO, AMENI.
Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

Na Huduma ya UKOMBOZI GOSPEL, Arusha Tanzania, Kwa Maombi, Ushauri, Maswali au Sadaka wasiliana nasi, Barua pepe: ukombozigospel@gmail.com  Simu: +255 759 859 287 pia waweza itumia kwa M-PESA. Zaidi www.ukombozigospel.blogspot.com   
Pia #Like #Penda Page/Ukurasa wetu au kundi la Fb, ili kupata habari hizi kwa haraka, zaidi. @ugukombozi Gospel  
 PAGE: https://www.facebook.com/ugukombozigospel/ 
Kikundi: https://www.facebook.com/groups/2268418230050621/ 
Pia kwenye mtando Mpya wakitanzania wa 
2 DAY SKY: https://www.2daysky.com/ukombozigospel  
 Pia TAZAMA VIDEO ZETU HAPA  https://www.youtube.com/channel/UCv1tghnugOSpbmb5h6ebJtA  (Ukombozi Gospel)
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba: Mahali wanafunzi wa Mkuu Sec School. 22/2/19. KISUDIO LA AKILI KIBIBLIA KATIKA KUKUFANIKISHA KIMAISHA.


Mithali 3:19 Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya nchi; Kwa akili zake akazifanya mbingu imara;
Fahamu: Kukosa Akili, au kushindwa kuitumia Akili, huwa na madhara kadha wa kadha:

1. Kutapanya Mali, au Kushindwa kuthamini chenye thamani; Mithali 11:22 Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe, Kadhalika mwanamke mzuri asiye na akili.
Unampeleka shule, anaanza kuvuta bangi, anajiingiza kwenye ukahaba, na makundi hatarishi, uwe na uhakika ni pete yenye thamani ya dhahabu ila imo kinywani mwa nguruwe, yaani kapewa elimu, ila hana akili ya kuithamini, ataichezea na kuiharibu.

2. Uvivu; Mithali 24:30 Nalipita karibu na shamba la mvivu, Na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili.
31 Kumbe! Lote pia limemea miiba; Uso wake ulifunikwa kwa viwawi; Na ukuta wake wa mawe umebomoka.
32 Ndipo nilipoangalia na kufikiri sana; Naliona, nikapata mafundisho.
33 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, Bado kukunja mikono upate usingizi!

Biblia inatuambia kuwa uvivu ni tatizo la kutokutumia akili, kwa hiyo, ukimuona mwanafunzi hasomi, au ni mvivu kujisomea,ni mzito kuamka usiku, uwe na uhakika kuwa huyu anaitwa hana au atumii akili, au anatatizo katika akili yake, ikiwa na mantiki kuwa kazi moja wapo ya akili ni kuachilia msukumo wa uhodari na ufanyaji kazi kwa bidii katika masomo au katika kufanikisha usomaji wa mwanafunzi.

3. Dharau ni Dalili ya Mtu Asiye na Akili;  Mithali 11:12 Asiye na akili humdharau mwenziwe; Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.
Mwanafunzi asiye sikiliza wazazi wake, asiye sikilizawalimu, vio gozi wake, mwenye majigambo na kudharau wenzake, au kujiona ni mwenye thamani kuliko wengine, huyu kibiblia huitwa ni mwenye shida katika kuzitumia akili zake, maana kitu kimoja wapo ambapo akili imepewa ni ili iweze kutengeneza umoja, nithamu, utii, uadilifu, na mshikamano, ndiposa sisi tu tofauti na wanayma, isimizi wanaosifuwa na Mithali, kwamba ni wenye akili, sifa yao moja ni umoja. Sasa penye dharau hakuna umoja, bali pana kujitenga, na kubagua wengine.
Muhimu: Akili ukizitumia vibaya nazo hutumka:

Ikupe kuepuka kutumia akili zako ili kubuni vitu vitakavyo potosha watu zaidi, vitu vitakvyo zidi kuiangamiza jamii, vitu vitakavyo tumika kama silaha ya dhambi, pia kwa akili zako usizitumie kutongozea, au kushawishi wengine ili uzini nao, maana Mithali sita husema huyu hana akili kabisa, wapo wanafunzi wanaozitumia akili zao vibaya, hili ni tatizo katika vitabu vyetu,nimeweka onyo la kuathibiwa, na andiko nikupalo linasema kuwa huyu hana akili, A hiyo hunui kusema kwamba hana kili katika kumjua Mungu, maana amjuaye Mungu hutamani kumpendezesha Yeye, lakini B yake husema kuwa ana akili katika kutenda mabaya ikiwa na maana kwamba, huzitumia akili zake alizopewa na Mungu vibaya, aidha za kuzaliwa kama kipaji ama kipawa, ama uelewa mkubwa zaidi aliopewa. Nia ya pwenti hii ni kukutaadharisha katika matumizi mabaya ya upeo mkubwa uliopewa na Mungu, Paulo Mtume alipewa na hapo awali aliitumia vibaya, akalitesa kanisa,baadae akaja kugundua siri na kuja kuutumia vizuri zaidi katika kuliimarisha, sasa wewe ujumbe huu sii wa bahati mbaya kwako bali ukusukume katika kuzitumia ili uujenge ufalme wa Mungu, mie natumia zangu kuhubiri injili, kuandika vitabu, na kukupasha jumbe kama hizi, zamani nilianza kuzitumi vibaya kwa kutunga Filamu na Hadhithi, ila sasa nazielekeza msalabani ! Wewe je? Umepewa kuimba, au kupiga ala za Muziki, jiulize unapiga katika Bwana au katika Lusifa! Unaimba nyimbo zakumuimbia Mungu au Shetani? 

Yeremia 4:22 Kwa maana watu wangu ni wapumbavu, hawanijui; ni watoto waliopungukiwa na akili, wala hawana ufahamu; ni wenye akili katika kutenda mabaya, bali katika kutenda mema hawana maarifa.
Utendaji wa Akili:

1. Ndani ya Kipawa au Kipaji Kuna Akili;
Kutoka 35:31 naye amemjaza roho ya Mungu, katika hekima, na akili, na ujuzi, na kazi ya ustadi kila aina;
:35 Amewajaza watu hao akili za moyoni, ili watumike katika kazi kila aina, ya mwenye kuchora mawe, na kazi ya werevu, na ya mwenye kutia taraza, katika nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri, na ya mwenye kufuma nguo; ya hao wafanyao kazi yo yote, na ya wenye kuvumbua kazi za werevu.

Kwa hiyo, uimbaji ni akili za uimbaji, muandisi, mkemia ama mwanabaolojia ni akili katika alichokisomea,kiongozi ana akili za uongozi, hii ikupe kukaa vyema kwenye karama na kipawa ulichopewa na Mungu, ili utumie kwa utukufu wake.

2. Akili Kidhiirika katika Utendaji Ndipo huweza kukusaidia, ile una akili lakini hauitumi, ni sawa na kuwa na umeme usioutumika, ni sawa na mtu mwenye maji ila hayatumii, kiu haiondoki kwa kuwa na maji, bali kwa kuyanywa, na ufahamu kuwa huwezi kuyanywa kama huna, kwa hiyo kuwa nayo ni muhimu, kisha kuyatumia pia.
Yusufu alikuwa na akili ila yupo jela, alipotoka, akili yaje ikadhiirika, hii ikupe kujiombea ili kujitoa kwenye vifungo vikamatavyo akili, kama kufungwa fahamu na kadhalika.

Kuna wanafunzi waliwekwa jela za kuvuta bangi, jela za uzinifu, jela za kiburi, na kila tabia hatarishi ikiwemo ya kutokutii ama kuheshimu wazazi wao na walimu, huyu ujuwe adui ananuia kuzizuilia akili zake zisiwe na matunda maana hazipo katika utendaji, akiadhibiwa kusimamishwa shule, ama kukosa utulivu wa kujisomea kwa sababu ya hizo tabia, uwe na uhakika,akili yake, haiwezi kukua, maana maarifa ya darasani ndiyo ya kuzayo akili yake!

Tujionee kwa Yusufu; Mwanzo 41:12 Na huko pamoja nasi palikuwa na kijana; Mwebrania, mtumishi wa mkuu wa askari, tukamhadithia, naye akatufasiria ndoto zetu; akamfasiria kila mtu kama ilivyokuwa ndoto yake.

Ni mujiza pekee ndio ulitengeneza mwanya wa akili zake kuanza kuchanua akiwa jela; 

Baada ya kutoka Jela, ndipo matunda ya akili yake hujidhiirisha, kwanza jionee utendaji wake; 
Mwanzo 41:39 Farao akamwambia Yusufu, Kwa kuwa Mungu amekufahamisha hayo yote, hapana mwenye akili na hekima kama wewe.

Matunda: Mwanzo 41:40 Basi wewe utakuwa juu ya nyumba yangu, na kwa neno lako watu wangu watatawaliwa. Katika kiti cha enzi tu nitakuwa mkuu kuliko wewe.

3. Hukupa Kujiwekea Akiba ya Maarifa; 
Mithali 10:14 Watu wenye akili huweka akiba ya maarifa; Bali kinywa cha mpumbavu ni uangamivu ulio karibu.
Kwa hiyo,mwanafunzi mwenye akili, hujituma katika kujisomea.
4. 

NB: Akili zinahesabika, au kupimika, kwa hiyo, muombe Mungu akuongezee kama una huo uhitaji:
Lakini kabla ya kuongezewa au kuyaomba hayo, hakikisha ulizo nazo zinatumika vizuri, au unuie kuzitumia vizuri, pili hakikisha unazifungua, au kuzikomboa ulizo nazo, kama kuomba moyo wa ufahamu na kukomboa fikra zako kwa Damu ya Yesu.

1 Wafalme 4:29 Mungu akampa Sulemani hekima, na akili nyingi sana, na moyo mkuu, kama mchanga ulioko pwani.
Mithali 30:24 Kuna viumbe vinne duniani vilivyo vidogo; Lakini vina akili nyingi sana.

Zekaria 9:2 na Hamathi pia iliyo mpakani mwake; na Tiro, na Sidoni, kwa maana ana akili nyingi.
Zekaria 9:3 Na Tiro alijijengea ngome, akakusanya fedha kama mchanga, dhahabu safi kama matope ya njia kuu.
Fahamu Sana: Asiye na Akii, au Asiyetumia Akili, ama Ambaye akili zake zimefungwa, au kuzuiliwa, huwa mzito kuelewa; 
Mathayo 15:14 Waacheni; hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote wawili.
15 Basi Petro akajibu, akamwambia, Tueleze mfano huo.
16 Yesu akasema, Hata sasa ninyi nanyi mngali hamna akili?
17 Hamjafahamu bado ya kuwa kila kiingiacho kinywani hupita tumboni, kikatupwa chooni?
Kwa hiyo, Muombe Mungu azifunuliye akili zako ili zipate na kuelewa; 
Luka 24:45 Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko.
46 Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;
47 na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu.
48 Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya.
BWANA YESU, NIMETAMBUA KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NATUBU MBELE ZAKO LEO, NISAMEHE NA NINAKUOMBA UFUTE JINA LANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU, TAFADHALI LIANDDIKE KWENYE KITABU CHA UZIMA, NINAKUKIRII NA KUKUPOKEA MOYONI MWANGU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, HAKIKA WEWE NI MUNGU NA ULIFUFUKA KATIKA WAFU, Amen.

Hongera kwa kuokoka na tafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo, kwa maombi, sadaka kwa njia ya M-Pesa, kupiga simu au Wasats App, ni +25559859287. Tupo Arusha Tanzania.
0 Toa maoni yako.

The Ug Tv Yaja PUNDE, IS COMING SOON

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

MWALIMU OSCAR SAMBA SABABU ZA KUTOA SADAKA NA MAJIBU YAKO KUCHELEWA KIBI...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

NAFASI YA SADAKA KATIKA KUKUWEZESHA KUTIMIZA MAONO AU NDOTO ZAKO

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba MSIKILIZE MUNGU

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba, Mbinu Teule za Kutoka Kwenye Umasikini Kwa Watu Wal...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba, Mbinu Teule za Kutoka Kwenye Umasikini Kwa Watu Wal...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba, Mbinu Teule za Kutoka Kwenye Umasikini Kwa Watu Wal...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba, Mbinu Teule za Kutoka Kwenye Umasikini Kwa Watu Wal...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba, Mbinu Teule za Kutoka Kwenye Umasikini Kwa Watu Wal...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba, Mbinu Teule za Kutoka Kwenye Umasikini Kwa Watu Wal...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba, Mbinu Teule za Kutoka Kwenye Umasikini Kwa Watu Wal...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.
HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

Mwalimu Oscar Samba, Mbinu Teule za Kutoka Kwenye Umasikini Kwa Wtu Wali...

HABARI ZETU
0 Toa maoni yako.

THE LITERATURE OF TEACHER JOHN LUOGA AT TAG CHURCHIPLANTING IN MAKUYUNI ...

MWALIMU WANGU JOHN LUOGA KATIKA CHUO CHA BIBLIA TAG ARUSHA KILICHOPO MAKUYUNI AKITUFUNDISHA, mie ni mpiga picha na sifa yetu kubwa hatuonekanagi so usishangae usiponiona
0 Toa maoni yako.
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company