Kikosi cha AU chakomboa mji CAR


Kamanda wa kikosi cha amani cha Umoja wa Afrika katika Jamhuri ya Afrika ya Kati anasema askari wake wameukomboa mji wa Sibut, kutoka kwa wapiganaji wa zamani wa Seleka.
Kamanda huyo, Jenerali Tumenta Chomud, alisema askari kutoka Gabon sasa wako mjini Sibut, na watawanyang'anya silaha wapiganaji waliouteka mji huo Alkhamisi.

Wapiganaji wa zamani wa Seleka - wengi wao Waislamu - wamekuwa wakiondoka mji mkuu, Bangui, ambao uko kama kilomita 200 kusini ya Sibut.

Kuondoka kwa Seleka kumezusha mauaji ya kulipiza kisasi, na watu zaidi ya 40 wameuwawa mjini Bangui katika siku chache zilizopita.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company