Posho juu bungeni Ikulu, Bunge wazunguka mbuyu

WAKATI Ikulu ikitangaza kuwa posho kwa wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba haijaongezeka, Tanzania Daima imebaini kuwa imeongezeka kwa sh 140,000 kwa siku za Jumamosi na Jumapili tofauti na ilivyokuwa siku za nyuma.
Kuongezeka kwa posho hiyo ingawa kihesabu imebaki vilevile sh 300,000 kwa siku kunatokana na Ikulu kubariki pendekezo la uongozi wa Bunge Maalum la Katiba kutaka posho ya kujikimu ambayo ilikuwa sh 80,000 iwe posho ya kikao na ile ya kazi maalumu ya sh 220,000 iwe posho ya kujikimu.
Kabla ya mageuzi hayo, siku za Jumamosi na Jumapili wajumbe walikuwa wakilipwa sh 80,000 kama posho ya kujikimu, lakini kuanzia sasa watalipwa sh 220,000 ambayo imegeuzwa kuwa posho ya kujikimu na ile 80,000 iliyokuwa ya kujikimu imegeuzwa kuwa ya kikao.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company