Raia Nigeria wapinga posho za wabunge

Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria

Wananchi wa Nigeria wamechukizwa na taarifa kwamba wabunge wamejiidhinishia mamilioni ya dola kwa ajili ya posho ikiwemo ya mavazi.

Gazeti moja nchini Nigeria limesema kuwa kwa mujibu wa sheria ya posho inayohusisha pia kipengele cha mavazi, kila mjumbe wa baraza la Seneti na Baraza la Wawakilishi atapokea wastani wa dola za Kimarekani laki moja katika mhula mmoja wa kipindi cha miaka minne.

Umaskini umetapakaa nchini Nigeria kwa idadi ya watu milioni mia moja wa Nigeria wakishi maisha ya chini ya dola moja kwa siku. Ujumbe mwingi umetumwa katika mitandao ya kijamii ukipinga malipo hayo.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company