Na Ibrahim Yamola na Peter Saramba, Mwananchi
Dar/Arusha. Jeshi la Polisi Zanzibar limeendelea kuuchelewesha mkutano wa wanachama wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kwa madai kwamba hakuna askari wa kutosha kuulinda.
Mwenyekiti wa Ukawa, Freeman Mbowe alisema mkutano huo utafanyika leo katika uwanja huo. PICHA|MAKTABA
Awali, mkutano huo ulipangwa kufanyika Jumamosi iliyopita kwenye Uwanja wa Kibandamaiti, Unguja lakini jeshi hilo liliuzuia kwa madai ya kuwapo kwa habari za kiintelijensia dhidi ya tishio la maisha ya watu.
Awali, Mwenyekiti wa Ukawa, Freeman Mbowe alisema mkutano huo utafanyika leo katika uwanja huo.
Ukawa ni muungano wa vyama vya Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi, DP na wajumbe 25 kutoka kundi la wajumbe 201 walioteuliwa na Rais Jakaya Kikwete.
Hata hivyo, Msemaji wa Polisi Zanzibar, Mohamed Mhina alisema baadaye kuwa mkutano huo hautafanyika hadi Aprili 30, mwaka huu.
Alisema umezuiwa kwa sababu askari na maofisa wa polisi wanaotakiwa kuusimamia wako Dar es Salaam katika maandalizi ya sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
“Tumekutana nao (CUF walioomba kibali kwa niaba ya Ukawa) na kukubaliana kwamba mkutano huo ufanyike Aprili 30 kwani askari waliopo hivi sasa ni wachache hawawezi kutosha kusimamia ulinzi kutokana na aina ya mkutano wenyewe. Hata hiyo siku hiyo hakutakuwapo na maandamano, bali wataruhusiwa kufanya mkutano pekee na siyo vinginevyo.”
TAIFA STARS HAZARANI
-
Kaimu kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Etiene Ndairagije ametangaza
kikosi cha timu ya taifa chenye wachezaji 30 ambao wanajiaandaa na mchezo
wa kuwania ...
5 years ago