Mh. Lowasa baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mpanda na kupata mapokezi kishindo na wadhamini zaidi ya elfu tatu aliwashukuru wote waliompokea na kuwataka kuendelea kuhamasishana kujiandikisha na baadaye kupiga kura muda ukifika.
Awali mwenyekiri wa CCM wa mkoa wa Katavi Bw Mselem Saidi Abdllah aliwataka wanaccm kote nchini kuwatendea haki wagombea wote wanaotafuta wadhamini kwani kwa vyovyote vile mmoja wao ndiye atakayekuwa kiongozi wao.
Lowasa ambaye pia jana alitembelea mkoa wa Rukwa na kupata wadhamini wengi, leo ataendelea kutafuta wadhamini katika mkoa wa Kagera.



