Wanasayansi China watumia nguruwe kutibu upofu

Wanasayansi wa Uchina wamefaulu katika tiba yao mpya ya majaribio ya kutibu upofu.

Walitumia nguruwe katika majaribio hayo ya tiba ya kuondoa upofu, ambapo walitumia konea kutoka kwa wanyama hao.

Sasa wamesema wana imani kwamba hilo litafaa sana kutokana na uhaba wa konea za binadamu.

Inakisiwa kuwa Wachina wapatao 5 milioni wanakabiliwa na matatizo ya konea, sehemu ya mbele ya jicho iliyo ngumu na inayowezesha miali ya mwanga kupenya.

Lakini ni konea 5,000 pekee ambazo hupatikana kila mwaka.

Matatizo ya konea husababisha watu wengi kuwa kipofu.Image copyrightGETTY

Njia hiyo mpya ya kutibu upofu imeanza kutumiwa baada ya kuidhinishwa na serikali mwaka jana.

Konea kutoka kwa nguruwe hutibiwa na kutolewa bakteria na virusi, pamoja na kutolewa DNA ya nguruwe, kabla ya kupandikizwa katika jicho la mwanadamu.

Wakosoaji wa mpango huo wanasema Uchina inaenda kwa kasi sana, bila kuangazia madhara ya mpango huo kwa kipindi kirefu
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company