WWF:Mbuga ya Selous Tanzania kupoteza Tembo wake

Rushwa ni moja ya sababu iliyochochea vita dhidi ya ujangili kutokwisha

Hifadhi ya wanyama pori ya taifa ya Selous Kusini mwa Tanzania inatajwa kuwa huenda ikapoteza tembo waliosalia ndani ya miaka sita ijayo iwapo hali ya ujangili itaendelea kwa kiwango kilichopo sasa.

Ripoti ya mfuko wa hifadhi ya wanyamapori na mazingira duniani,wwf imesema hifadhi Selous imepoteza asilimia tisini ya tembo wake,ambapo miaka 40 iliyopita kulikuwa na maelfu ya tembo.

Mahitaji makubwa ya nyara hizo na nchi ya China,kwa mjibu wa ripoti hiyo inatajwa kuwa ni hali inayochochea ujangili na mauaji ya idadi kubwa ya tembo.

Rais wa awamu ya tano wa Tanzania John Pombe Magufuli katika utawala wake ametanga kukomesha rushwa ambayo ndiyo imekuwa ikichangia kukua kwa vitendo vya ujangili.

"hifadhi hiyo ya Selous ni moja kati ya urithi wa dunia kufuatia kuwa na eneo kubwa la wanyama pori lililosalia Barani Afrika.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company