Ndege zisokuwa na rubani zatumika Mali

Marekani inatumia ndege za ujasusi zisokuwa na rubani kuwasaidia wanajeshi wa Ufaransa na Umoja wa Afrika kupigana na wapiganaji wa Kiislamu wa Mali.
Mapigano nchini Mali
Afisa mmoja wa jeshi la Marekani alieleza kuwa ndege hizo, yaani drones, hazitakuwa na silaha na zitaongozwa na wanajeshi kama 100 wa Marekani kutoka nchi jirani, yaani Niger.
Hatua hiyo inafuatia juhudi za Marekani za kupambana na wapiganaji wenye uhusiano na Al Qaeda kaskazini na magharibi mwa Afrika.
Chad inasema kuwa wanajeshi wake wamekuwa wakipambana vikali na wapiganaji katika eneo la milima kaskazini mwa Mali.
Inaarifiwa kuwa wapiganaji kama 65 na wanajeshi 13 wa Chad wameuwawa.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company