Polisi
nchini Brazil inawashikilia watu wanne kwa tuhuma za kuhusika na tukio
la moto uliosababisha vifo vya watu 231 katika klabu ya usiku kwenye mji
wa Santa Maria Kusini mwa nchi hiyo hapo juzi.
Miongoni mwa watu hao ni mmiliki wa klabu hiyo ambaye amehojiwa kwa masaa kadhaa na polisi.
Zaidi ya watu hamsini wamezikwa jana huku serikali ikitangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa
