Afa kwa kujilipua na petroli

na Ahmed Makongo, Bunda

KULWA Mirobho (39), maarufu kwa jina la Jogoo la Mara, mkazi wa Kijiji cha Nambaza wilayani Bunda amekufa baada ya kulewa pombe na dawa za kulevya kisha kujimwagia mafuta aina ya petroli mwili mzima na kujilipua moto. Mwenyekiti wa Kijiji cha Nambaza, Alfred Taganga alisema tukio hilo lilitokea kijijini kwake Machi 5, mwaka huu majira ya saa 11:00 jioni.
Alisema kuwa mwanaume huyo baada ya kutumia dawa za kulevya aina ya bangi na pombe aina ya gongo, alichukua mafuta ya petroli yaliyokuwa yanauzwa kwenye kituo kijijini hapo na kujimwagia mwili mzima na kisha kuwasha kibiriti na kujilipua kwa moto.
Ilielezwa kuwa baada ya kujilipua kwa moto alianguka chini na ndipo wananchi wakammwagia mchanga ili wauzime moto huo. Baada ya kufanikiwa kuuzima walimpeleka hospitali.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Misheni Kibara, Dk. Cosmas Fabian alisema mwanaume huyo alifariki dunia kesho yake majira ya saa 12:00 asubuhi, kutokana na kupata majeraha makubwa yaliyosababishwa na moto huo.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company