
Raisi Jakaya M. Kikwete akiwasili kwenye uwanja wa Taifa wa Uhuru ili kuwaongoza watanzania katika maadhimisho ya miaka 52 ya uhuru wa Tanganyika. Tanganyika ilipata uhuru mwaka 1961 tarehe 9 Desemba. Watanzania wengi wamekusanyika kwenye uwanja wa Uhuru ili kuweza kuungana na watanzania wengine katika maadhimisho haya.