Ni rasmi - Mkataba wa amani DRC na M23


Bertrand Bisimwa akisaini mkataba jijini Nairobi
Serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo hatimaye imesaini mkataba wa amani na waasi wa kundi la M23 waliokuwa wakifanya mashambulio ya mara kwa mara mashariki mwa nchi hiyo.
Waasi wa M23 walijilsalimisha mwezi uliopita baada ya kushindwa katika oparesheni iliyoendeshwa na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ikisaidiwa na majeshi ya Umoja wa Mataifa. Alhamisi, marais Yuweri Museveni, ambaye ndiye mwenyekiti wa kongamano la kimataifa juu ya usalama katika maziwa makuu, na Joyce Banda, rais wa Malawi, ambaye ndiye mwenyekiti wa jumuiya ya maendeleo ya kusini mwa Afrika SADC, walisaini kama wadhamini wa mkataba huo.


Marais hao walisaini mkataba huo wakiwa jijini Nairobi walikohudhuria sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru wa Kenya.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company