Tunisia:Tumechoshwa na serikali



Wengi wanasema serikali inajikokota kupiga hatua tangu mapinduzi ya kiraia

Maelfu ya watu nchini Tunisia wamekuwa wakifanya maandamano mjini Sidi Bouzid, kitovu cha harakati za mapinduzi ya kiraia yaliyomwondoa mamlakani aliyekuwa Rais Zine el-Abidine Ben Ali miaka mitatu iliyopita.
Waandamanaji wanalalamikia ukosefu wa serikali kupiga hatua za kuridhisha tangu mapinduzi ya kiraia kufanyika.

Mji wa Sidi Bouzid ndiko kijana mmoja mchuuzi Mohamed Bouazizi alijiteketeza miaka mitatu iliyopita kuonyesha ghadhabu kwa ambavyo serikali ilikuwa inawanyanyasa raia wake.

Maandamano yaliyofuata tukio la kijana huyo kujiua, yalimwondoa mamlakani aliyekuwa Rais Zine el-Abidine Ben Ali na kuchochea maandamano mengine kama hayo katika nchi za kiarabu.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company