Hofu ya UNHCR kuhusu wakimbizi Wasomali Kenya

Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Wakimbizi UNHCR limeelezea wasi wasi wake kuhusu kutiwa mbaroni idadi kubwa ya wakimbizi Wasomali katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi.

Katika taarifa, UNHCR imesema wakimbizi Wasomali wanaoshikiliwa wanapaswa kulindwa na kutokamatwa kiholela. Waziri wa Mambo ya Ndani wa Kenya Joseph Ole Lenku amenukuliwa akisema zaidi ya watu 4,000 wamekamatwa katika siku za hivi karibuni. Kati ya wanaoshikiliwa katika oparesheni ya vikosi vya usalama Kenya ni zaidi ya Wasomali 1,000 ambao imeripotiwa wanazuiliwa katika uwanja mmoja wa michezo mjini Nairobi. Kuna ripoti kuwa waliokamatwa hawana chakula, maji na dawa katika uwanja huo. Vikosi vya usalama Kenya vinatekeleza oparesheni kubwa ya kiusalama yenye lengo la kuwasaka magaidi kufuatia hujuma za kigaidi katika miji ya Nairobi na Mombasa. Kundi la kigaidi la Al Shabab limenukuliwa mara kadhaa likisema litatekeleza hujuma Kenya kulipiza kisasi uingiliaji wa jeshi la Kenya nchini Somalia. Wanajeshi wa Kenya wako Somalia kama sehemu ya Vikosi vya Kulinda Amani vya Umoja wa Afrika (AMISOM) ambavyo viko Somalia kupambana na kundi la al-Shabab.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company