Ukrain kujibu mapigo

Mwanajeshi wa Ukrain

Jeshi la Ukrain limeanza kujihami mashariki mwa nchi hiyo dhidi ya mashambulizi ya waasi wa Urusi kufuatia kutunguliwa kwa ndege ya Malaysia katika eneo hilo.

Msemaji wa serikali ya Ukrain Andriy Lysenko amesema jeshi la nchi hiyo lilidhamiria kulifunga eneo hilo ili kupisha uchunguzi wa watalaamu kuhusiana na chanzo cha kuanguka kwa ndege hiyo.

Ndege ya Malaysia iliyokuwa imebeba watu 300 iliangushwa katika eneo hilo lililo chini ya udhibiti wa waasi.

Waangalizi wa kimataifa wanasema mapigano hayo yataadhiri uchunguzi wa ajali hiyo ya ndege, mapigano makali yameripotiwa katika amaeneo yanayozunguka mji wa Horlivka na Shakhtarsk.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company