Vifo vinavyotokana na ugonjwa wa Ebola vyaongezeka Sierra Leone,Liberia

 
Wahudumu wa afya huko Magharibi mwa Afrika wakitoa huduma kwa waathirika wa virus vya Ebola
AFP PHOTO / SEYLLOU

Na RFI
Idadi kubwa ya ripoti mpya za maambukizi ya virusi vya Ebola imetajwa huko Sierra Leone na Liberia ambapo kumearifiwa vifo 19 kutokea ndani ya siku tatu za juma hili,shirika la afya duniani WHO limearifu.

Idadi hiyo inaonesha kwamba ni harakati dhidi ya muda wa kudhibiti ugonjwa huo huko Sierra Leone, wameeleza madaktari wasio na mipaka.

Kwa ujumla kumetokea vifo 539 huko Afrika Magharibi tangu kutokea kwa ugonjwa huo katika taifa jirani la gine mnamo mwezi wa pili.

Viongozi katika ukanda huo wamekubaliana kuchangisha fedha kwa ajili ya kukabiliana na kuenea kwa ugonjwa huo.

Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company