Baraza la Usalama lasikitishwa na Sudan Kusini

Wanajeshi watoto wa Sudan Kusini
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limelezea kusikitishwa kwake kutokana na rais wa Sudan Kusini, na kiongozi wa waasi Riek Machar kusindwa kufikia makubaliano ya amani.

Katika taarifa iliyotolewa na baraza hilo Jumanne, kwa mara nyingine tena imetishia vikwazo dhidi ya maafisa wa juu ambao inahisi wanawajibika na vitendo ama sera ambazo zitatishia amani, usalama, ama uthabiti ndani ya Sudan Kusini.

Mapigano katika taifa hilo tajiri la mafuta la Afrika Mashariki, yamesababisha vifo vya maelfu ya watu na kukosesha makazi zaidi ya watu milioni mbili.

Marekani, na Umoja wa Ulaya tayarri zimeshawawekea vikwazo makomanda wqa pande zote mbili.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company