Mahakama nchini Misri
Mahakama ya Misri imewahukumia kifungo ncha maisha jela, watu 69 baada ya kupatikana na hatia kuchoma kanisa moja nchini humo.
Kanisa hilo liliteketezwa moto wakati machafuko yalipozuka eneo la Kerdasa karibu na mji wa Cairo mwaka 2013.
Makabiliano makali yalizuka pale jeshi lilipoanza kuwaondoa wafuasi wa aliyekua Rais Mohammed Morsi kutoka maeneo waliokua wakiandamana.
Mamia ya waandamanaji waliuawa kwenye operesheni hiyo.
TAIFA STARS HAZARANI
-
Kaimu kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Etiene Ndairagije ametangaza
kikosi cha timu ya taifa chenye wachezaji 30 ambao wanajiaandaa na mchezo
wa kuwania ...
6 years ago

