Bei za vyakula zapaa, mfumuko wa bei mwezi Machi wafikia asilimia 4.2

Bidhaa za vyakula katika moja ya masoko nchini.
Picha ya mtandao. 

Na Suzan Mwillo, Mwananchi
KWA UFUPI
Upandaji wa bei za bidhaa hizo zimesababisha mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwezi iliyopita kuongezeka hadi ukufikia asilimia 4.3 kutoka asilimia 4.2 ya mwezi Februari mwaka huu.

Dar es Salaam. Upungufu wa chakula kwa baadhi ya mikoa nchini umeendelea kusababisha ongezeko la mfumuko wa bei wa Taifa kutoka asilimia 4.2 hadi asilimia 4.2 ndani ya mwezi mmoja.

Mkurugenzi wa Takwimu za Jamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Ephraimu Kwesigabo, aliwaambia waandishi wa habari leo kuwa, kutokana na upungufu huo bei za bidhaa za vyakula zimeongezeka.

“Mfumuko wa bei wa Taifa kwa kipimo cha mwaka unapimwa kwa kiwango cha badiliko la kasi ya bei za bidhaa na huduma zote zinazotumiwa na kaya binafsi,”alisema.

Aliongeza: “Hivyo kutokana na ongezeko la bei za bidhaa hizo pamoja na huduma zote kwa kaya zimesababisha mfumuko wa bei wa taifa,”alisema Kwesigabo.

Aliendelea kueleza kuwa, kasi ya upandaji wa bei za bidhaa hizo zimesababisha mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwezi iliyopita kuongezeka hadi ukufikia asilimia 4.3 kutoka asilimia 4.2 ya mwezi Februari mwaka huu.

Kwesigabo alisema, ongezeko la mfumuko wa bei kwa mwezi Machi umesababishwa hasa na kuongezeka bei za bidhaa za vyakula kwa kipindi kilichoishia Machi mwaka huu tofauti na ilivyokuwa kwa Machi mwaka jana.

Alizitaja bidhaa hizo kuwa ni pamoja na mchele, unga wa muhogo, nyama, samaki, maharage, choroko na sukari.

Alisema kutokana na hali hiyo wananchi wataendelea kushuhudia bei za vyakula zikiendelea kupanda na kwamba bei waliyokuwa wakinunua bidhaa za vyakula hapo awali itabadilika.

Akizungumzia thamani ya shilingi ya Tanzania kwa mwezi uliopita ikilinganishwa na mwezi Septemba, 2010 alisema, uwezo wa Sh 100 katika kununua bidhaa na huduma umefikia Sh 64 na senti 15 mwezi Machi mwaka huu kutoka Septemba, 2010.

“…ikilinganishwa na Sh 64 na senti 59 ilivyokuwa Febriari mwaka huu,”alisema Kwesigabo.

Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company