Wahamiaji wanaoelekea Italy
Mkuu wa utawala wa waasi nchini Libya ameiambia BBC kuwa vikosi vyao vinafanya juhudi ziwezekanazo kuzuia wahamiaji haramu kuabiri meli kuelekea Ulaya .
Khalifa Al-Ghwell - ambaye serikali yake ya uokozi yenye makao yake mjini Tripoli haitambuliwi kimataifa anasema walinzi wa Libya wa mwambao wamekuwa wakiwashikilia karibu wahamiaji mia nne - kutoka nchi za Sahara barani Afrika katika kipindi cha siku chache zilizopita .
Bwana Ghwell amesema kuwa wahamiaji elfu 17 walikuwa wanaishi katika kambi ya hifadhi nchini Libya , lakini ni asilimia karibu tano walioweza kuvuka na kuingia Ulaya.
TAIFA STARS HAZARANI
-
Kaimu kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Etiene Ndairagije ametangaza
kikosi cha timu ya taifa chenye wachezaji 30 ambao wanajiaandaa na mchezo
wa kuwania ...
5 years ago