Warren Weinstein
Ikulu ya Marekani imetangaza kuwa watu wawili waliokuwa wamezuiliwa na wapiganaji katika nyumba moja nchini Afghanistan, waliuwawa kimakosa na majeshi ya Marekani yanayopambana na ugaidi katika maeneo ya Afghanistan na Pakistan.
Akisoma taarifa kuhusiana na vifo hivyo, Rais Barrack Obama, amesema kuwa amesikitishwa mno na kisa hicho kilichofanyika Januari mwaka huu.
Anasema watu hao walikuwa wamezuiliwa na wapiganaji wa al Qaeda, kwa miaka kadha.
Wametajwa kama Mmarekani Warren Weinstein, na Giovanni Lo Porto raia wa Italia.
White House inasema pia kuwa, raia wengine wawili waliouliwa walikuwa waamerika, na wanachama wa kundi la al Qaeda.
TAIFA STARS HAZARANI
-
Kaimu kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Etiene Ndairagije ametangaza
kikosi cha timu ya taifa chenye wachezaji 30 ambao wanajiaandaa na mchezo
wa kuwania ...
5 years ago