Polisi wa Italia
Polisi nchini Italia wanasema kuwa wamewakamata watu 18 wanaoshukiwa kuwa wanachama wa Islamic State kutoka nchini Afghanistan na Pakistan katika oparesheni kubwa ya kupambana na ugaidi.
Wanasema kuwa wawili kati ya washukiwa hao wanaaminiwa kuwa walinzi wa aliyekuwa kiongozi wa al-Qaeda Osama Bin Laden na wengine wanashukiwa kuhusika kwenye mashambulizi nchini Pakistan likiwemo shambulizi lililotokea kwenye soko la Peshawar.
Oparesheni hiyo ilikuwa imeendeshwa kwenye kisiwa cha Italia cha Sardina .
Polisi walisema kuwa kundi linalofanyiwa uchunguzi lilikuwa limewapangia wanachama wake kuingia nchini Italia wakiwa na vyeti vya kufanya kazi au kama watafuta hifadhi.
TAIFA STARS HAZARANI
-
Kaimu kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Etiene Ndairagije ametangaza
kikosi cha timu ya taifa chenye wachezaji 30 ambao wanajiaandaa na mchezo
wa kuwania ...
5 years ago