Wahamiaji wachanja mbuga kuelekea Ulaya

Image copyrightGetty ImagesImage captionWahamiaji wakielekea Ulaya

Maelfu ya Wahamiaji wanajaribu kuingia bara Ulaya.

Huku Umoja wa Ulaya ukiangalia uwezekano wa kuwashughulikia wale ambao tayari wapo huko.

Shirika la Umoja wa Mataifa la huduma kwa Wakimbizi limeanza kuwasaidia maafisa wa Ugiriki kuwapokea idadi kubwa ya wahamiaji wapya wanaowasili katika kisiwa cha Lesbos.

nchini Hungary nako, mamia ya wahamiaji walipita kwenye mistari ya polisi kwa nguvu na kuvuka mpaka wa kuingia Serbia.

Wito wa Ufaransa na Ujerumani wa kuwekwa kwa mifumo ya kisheria ya kugawana wakimbizi baina ya wanachama wa Muungano wa Ulaya umepingwa na serikali kadhaa.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company