Mlipuko wawaua 17 Maiduguri,Nigeria


Boko Haram limekiri kufanya shambulizi hilo
Watu kumi na saba wamefariki mwenye mlipuko wa bomu lililokuwa limetegwa ndani ya gari mjini Maiduguri Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
Kundi la wapiganaji wa kiisilamu Boko Haram, limekiri kufanya shambulizi hilo.
Kwa mujibu wa taarifa za jeshi mshukiwa mmoja amekamatwa.

Mlipuko huo ulitokea karibu na soko moja mjini humo. Walioshuhudia tukio hilo wanasema kuwa waliwaona watu wakitoroka kutoka eneo hilo nguo zao zikiwa na damu.

Kundi la Boko Haram, limekuwa likifanya mashambulizi ya mara kwa mara Kaskazini mwa Nigeria likiishinikiza serikali kukubali sheria za kiisilamu kutumika katika eneo hilo ambako wakazi wake wengi ni waumini wa kiisilamu.

Miili ilionekana ikiwa imetapakaa kote huku shahidi mmoja akiambia BBC kuwa alisikia mlipuko mkubwa uliofatiwa na milipuko mingine midogomidogo
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company