Museveni akataa kuidhinisha mswada tata



Moses raia wa Uganda anayeshiriki mapenzi ya jinsia moja akitafuta hifadhi nchini Marekani
Rais wa Uganda, Yoweri Museveni amekataa kuidhinisha mswada ambao ikiwa utaidhinishwa utatoa adhabu kali kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja.

Museveni amemuandikia spika wa bunge barua na kumkosoa kwa hatua ya kupitisha mswada huo Disemba mwaka jana bila ya kuwa na idadi ya kutosha ya wabunge.
Aidha Rais amesema kuwa Watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja ni watu wenye akili timamu na wanaweza kuokolewa kutokana na tabia hiyo.

Mswada huo unatoa adhabu kali kwa watu watakaopatikana na hatia ya kushiriki mapenzi ya jinsia moja ikiwemo kufungwa jela na pia ni uhalifu kwa mtu yeyote kukosa kuripoti visa vya mapenzi ya jinsia moja.

Mwandisi wa BBC mjini Kampala Cathrene Byaruhanga anasema kuwa mswada huo pia unapendekeza kuadhibiwa kwa watu wanaozungumzia maisha ya wapenzi wa jinsia moja bila ya kuwakashifu kwani wanaweza kufungwa jela.

Kwa mujibu wa gazeti la Monitor, Rais Museveni amesema kwamba mswada huo ulishinikizwa zaidi kupitishwa na wabunge licha ya kuwashauri kusubiri hadi serikali itakapoutathmini.

Rais anaelewa kwamba ikiwa atauidhinisha mswada huo na kuufanya sheria kutakua na ukosoaji mkubwa kutoka kote hali inatakayochangia baadhi ya nchi za kigeni kusitisha msaada kwa Uganda.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company