Muadhirika wa tukio la moto Dick Lulandala akiwa na rafiki yake Luka wakiangalia ofisi yake inayojihusisha na uchapishaji wa mabango , fulana baada ya kuteketezwa na moto ambapo hakuna hata kimoja kilichonusurika
Jeshi la polisi lilifanya kazi nzuri kwa kudhibiti mali zilizonusurika, hata hivyo kijana mmoja aliwekwa chini ya ulinzi kwa kujaribu kuiba
Kikosi cha zimamoto kikifanya kazi kwa bidii kudhibiti moto huo ingawa waliishiwa na maji..
Hapa iringa moto unaosadikiwa kuwaka kutokana na itilafu ya umeme umeteketeza mali katika jengo moja lililopo mtaa wa benbela gangilonga katika manispaa ya iringa .jengo hilo linalomilikiwa na Shirika la nyumba limezungukwa na ofisi pamoja na maduka ya bishara, Moto umesababisha madhara makubwa na ulizimwa na kikosi cha zimamoto kwa kushirikiana na wananchi , Ally Britoni ni mwenyekiti wa mtaa huo na ameieleza kwanza jamii na mjengwa blog kuwa moto ulianza kwa kuziona cheche majira ya saa nne kasoro za usiku lakini pia amewashukuru kikosi cha zimamoto iringa kwa kuitikia wito kwa haraka.Dick Lulandala ni swahiba yangu aliyekuwa katika hali ya huzuni kwa kuteketea kwa mashine za uchapishaji zenye gharama kubwa sana. Mjengwa blog na kwanza Jamii inawapa pole wote walioathiliwa na moto huo....By Edward Majura Sagin