Rais Omar al Bashir kupelekwa ICC?

Rais Omar al Bashir wa Sudan
Mahakama nchini Afrika Kusini imeahirisha kwa muda amri yake ya kumzuia rais wa Sudan Omar al Bashir, kuondoka nchini humo.

Mahakama itasikiliza kesi hiyo tena Jumatatu ili kuamua ikiwa Bwana al-Bashir atakabidhiwa kwenye mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai ICC kukabiliana na mashtaka ya uhalifu wa kivita na mauaji ya kimbari yanayomkabili au la.

Rais huyo wa Sudan amekuwa nchini Afrika kusini kuhudhuria kikao cha viongozi wa Umoja wa Afrika mjini Johannesburg. Waziri wa mambo ya nje wa Sudan, Ibrahim al-Ghandour, amesema Bwana al-Bashir atarejea Sudan baada ya mkutano huo. "Tupo hapa kama wageni na kualikwa na serikali ya Afrika Kusini. Naamini serikali ya Afrika Kusini itaweza kukabiliana na mahakama zake na yeyote anayejaribu kumzuia Rais Bashir kuondoka nchini hapa. Naweza kuwaambia Rais Bashir ataondoka kwa wakati kama ilivyokuwa imepangwa." anasema waziri huyo wa mambo ya nje wa Sudan.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company