Mgombea Ubunge Jimbo la Ludewa Kwa Tiketi ya CCM, Deo Filikunjombe Apita Bila KUPINGWA

Mgombea Ubunge katika Jimbo la Ludewa kwa tiketi ya CCM Bw. Deo Filikunjombe, amepita bila kupingwa wilayani humo baada ya Mgombea wa Chadema kushindwa kutimiza Masharti na Taratibu za Ujazaji wa Fomu.

Msimamizi wa Uchaguzi Wilaya ya Ludewa, Ndg. Wiliam Waziri amesema leo kuwa Mgombea wa Chadema ameshindwa kutimiza taratibu za ujazaji wa fomu hizo hivyo kukosa sifa ya kuwa Mgombea wa Ubunge.

Ndg. Waziri amesema kwamba Kati ya wagombea wanne waliochukua fomu aliyetimiza taratibu ni Mgombea wa CCM, Bw. Deo Filikunjombe pekee;

Wagombea wa DP na TLP waliishindwa kabisa kurejesha fomu huku Mgombea wa Chadema akishindwa kujaza fomu vizuri na kushindwa kurejesha Fomu ya Kiapo cha Maadili ya Sheria za Uchaguzi.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company