Salva Kiir akubali kutia sahihi ya amani

Image copyrightAFPImage captionSudan Kusini

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amesema kuwa ataweka sahihi ya makubaliano ya amani siku ya jumatano baada ya kukataa kufanya hivyo wiki iliopita.

Msemaji wa Salva Kiir amesema kuwa rais huyo ataweka sahihi yake ya makubaliano hayo katika mji mkuu wa Juba mbele ya viongozi wa eneo hili.

Salva Kiir anakabiliwa na vikwazo pamoja na kikwazo cha umoja wa mataifa cha kutonunua silaha baada ya kukataa kuidhinisha makubaliano hayo.

Mpinzani wake ambaye ndio kiongozi wa waasi Riek Machar tayari ameweka sahihi mkataba huo ili kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyochukua miezi 20.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company