Baada ya zoezi la upigaji kura kukamilika hapo saa 10 jioni, baadhi ya vituo vimeanza kuhesabu kura huku baadhi ya wakazi wa mkoa wa Mbeya wakiipongeza
Baada ya zoezi la upigaji kura kukamilika hapo saa 10 jioni, baadhi ya vituo vimeanza kuhesabu kura huku baadhi ya wakazi wa mkoa wa Mbeya wakiipongeza Tume ya Uchaguzi ya Taifa –NEC- kwa maandalizi mazuri ya kufanikisha zoezi la upigaji kura licha ya kasoro ndogo zilizojitokeza katika baadhi ya maeneo.
Wakizungumza na TBC kwa nyakati tofauti wamesema zoezi la upigaji kura kwa mwaka huu limekuwa na mwamko mkubwa kwa wananchi hali inayoonyesha wengi wana elimu ya uraia.
Nako mkoani Dar es Salaam, TBC ilitembelea baadhi ya vituo na kushuhudia polisi wakilinda vituo hivyo wakati kura zikiwa zinahesabiwa huku kukiwa na hali ya utulivu na wananchi kutokuwepo katika maeneo hayo.
Baadhi ya kasoro zilizojitokeza katika jiji la DSM ni kutokuwepo kw amajina ya wananchi katika daftari la kudumu la kupigia kura walilokuwa nalo wasimamizi wa uchaguzi katika kituo cha shule ya MUGABE jimbo la UBUNGO hali iliyowafanya wapiga kura katika kituo hicho kukaa mpaka wakati wa kuhesabu kura wakiwa wanasubiri kujua hatma yao.
TAIFA STARS HAZARANI
-
Kaimu kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Etiene Ndairagije ametangaza
kikosi cha timu ya taifa chenye wachezaji 30 ambao wanajiaandaa na mchezo
wa kuwania ...
5 years ago