Mkurugenzi waNEC asema uchaguzi umefanikiwa kwa asilimia 99

Mkurugenzi wa Tume ya taifa ya uchaguzi -NEC RAMADHANI KAILIMA amesema wamefanikisha zoezi la upigaji kura kwa asilimia tisini na tisa kwa wapiga kura
Mkurugenzi wa Tume ya taifa ya uchaguzi -NEC RAMADHANI KAILIMA
Mkurugenzi wa Tume ya taifa ya uchaguzi -NEC RAMADHANI KAILIMA amesema wamefanikisha zoezi la upigaji kura kwa asilimia tisini na tisa kwa wapiga kura kupiga kwa amani na kurudi katika makazi yao ingawa kuna dosari katika kata za SUMBAWANGA na KINONDONI jijini DSM


Akizungumza baada ya baadhi ya vituo kuhitimisha zoezi hilo KAILIMA amesema huko SUMBAWANGA watu wasiojulikana waliliteka nyara gari lilolobeba vifaa vya uchaguzi na kuliteketeza kwa moto wakati katika kata ya KIMARA wilayani KINONDONI wafanyakazi wamechana karatasi za kura kwa kudai malipo zaidi

Naye Mkurugenzi wa huduma za sheria wa NEC EMMANUEL KAWISHE amesema Tume itaendelea kusimamia sheria za uchaguzi

Tume ya taifa ya uchaguzi imetoa angalizo kuwa hakuna mtu yeyote anayetakiwa kutangaza matokeo ya uchaguzi kuanzia ngazi ya udiwani hadi wa urais isipokuwa tume hiyo pekee.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company