AU kuendelea na mkutano wa Addis leo


Viongozi wa Afrika wakiwa katika mkutano wa AU, Addis Ababa Ethiopia
Viongozi wa Afrika wakiwa katika mkutano wa AU, Addis Ababa Ethiopia
Mkutano wa viongozi wa nchi za Umoja wa Afrika unaendelea leo mjini Addis Ababa Ethiopia baada ya kuvunjika hapo jana kwa makubaliano ya amani kuhusu mzozo wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Msemaji wa katibu mkuu wa umoja wa mataifa, Eri Kaneko, amesema kuwa suala la Congo ni zito na kwamba mazungumzo bado yanaendelea, ingawa hakutoa taarifa zaidi kuhusu uamuzi huo.
Ikiwa leo ni siku ya pili na ya mwisho ya mkutano huo, masuala kadhaa hasa yanayohusu migogoro iliyozikumba nchi za Afrika ikiwemo Mali, Sudan na Sudan Kusini pamoja na Jamuhuri ya Kidemocrasia ya Congo yataendelea kujadiliwa.
Pia suala la kutafuta fedha na vifaa kutoka Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kuvisaidia vikosi maalumu vya Umoja wa Afrika nchini Mali, na kupambana na wanamgambo wa Kiislamu.
Hapo jana Pande zinazohusika katika mgogoro huo wa DRC zilitarajiwa kutia saini mkataba wa amani lakini muda mfupi kabla ya tukio hilo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon akatangaza kuwa mazungumzo hayo yamevunjika.
Habari zinasema Afrika Kusini imegoma kuridhia mazungumzo hayo baada ya kutoridhika na maelezo yaliyotolewa na pande zinazohusika na mazungumzo hayo.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company