Watuhumiwa watano wanaodaiwa kushiriki katika kitendo cha kumkata mkono Mlemavu wa ngozi Albino Maria Chambanenje
Watuhumiwa
hao wamefikishwa mahakamani baada ya uchunguzi wa jeshi la
polisi kubaini walikuwa na mkono wa Albino huyo ambao walifukia
ardhini mara baada ya kuukata.
Watuhumiwa
hao wamefikishwa mahakamani hapo chini ya ulinzi mkali wa askari Polisi
na kusomewa mashtaka yao huku wakitakiwa kutojibu lolote, ambapo upande
wa Jamhuri ukiwashtaki kwa makosa mawili ikiwa ni pamoja na kosa la
kula njama ya kutaka kuua na kujaribu kuua.
Miongoni
mwa washtakiwa hao yupo Mume wa Albino huyo Gabriel Yohana, shemeji
yake Gaudensi Yohana, Mganga wa jadi Kaponda Muyamba, Mtuhumiwa wa
kutengeneza mchoro huo Linus Silukala na Mtuhumiwa aliyetaka kuununua
mkono huo Mtogwa Cosmas alimaarufu kama mzee wa Ishu mkazi wa Sokomatola
jijini Mbeya.
Hatahivyo
mahakama hiyo iliyokuwa chini ya Hakimu mkazi Mh. Rosalia Mugisa
imeweka wazi dhamana kwa watuhumiwa hao wote kwa pamoja huku mahakama
hiyo ikitoa masharti manne ya dhamana hiyo, ikiwa ni pamoja na kuwa na
wadhamini watatu wakazi wa wilayani Sumbawanga, fedha taslimu shilingi
milioni tatu kila mmoja, na mmoja wa wadhamini awe ni mwajiriwa wa
serikali au Shirika lolote la umma, ambapo washtakiwa hao walishindwa
maaelekezo ya dhamana hiyo na kurudishwa mahabusu hadi Machi sita
itakapotajwa tena.
