Hatufanyi kampeni Papa achaguliwe kutoka Afrika'

Papa Benedict XVI,
Alisema hayo alipokuwa akijibu maswali kutoka kwa waandishi wa
habari waliotaka kujua kama kuna uwezekano au mpango wa nafasi hiyo
kushikwa na kiongozi mmojawapo kutoka Afrika, hususan Askofu Mkuu wa
Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Polycarp Kardinali Pengo.
“Hatufanyi kampeni yoyote kwamba, Baba Mtakatifu atoke Afrika,
hususan Tanzania…hatufikirii hata mara moja kwa kigezo kwamba, atoke
Afrika,” alisema Askofu Lebulu.
Alisema kanisa hilo lina mifumo ya uchaguzi, ambayo ni tofauti na inayofanyika maeneo mengine.
Askofu Lebulu alisema mifumo yao ni ya kiroho na inayozingatia
miongozo ya kanisa, kama vile sala na kwamba, makardinali ndio
wanaomchagua Baba Mtakatifu.
Alisema kutokana na mifumo hiyo, hakuna anayepigania au kufanya
kampeni ili achaguliwe kuwa Baba Mtakatifu au kwa nafasi nyingine yoyote
ya uongozi katika kanisa hilo.
Askofu Mkuu Lebulu alisema hayo kufuatia uamuzi wa Papa Benedict
XVI, Februari 11, mwaka huu, kutangaza kujiuzulu mwishoni mwa mwezi huu
baada ya kuliongoza kanisa hilo kwa miaka minane.
Alitangaza uamuzi huo kwa hoja kuwa umri wake wa miaka 85 ni mkubwa kiasi kwamba, hawezi kuendelea kuhudumu zaidi ya umri huo.
