Kiongozi wa upinzani nchini
Misri, Mohammed ElBaradei, ametoa wito kuwa watu wasusie uchaguzi ujao
wa wabunge unaotarajiwa kufanywa mwezi ujao.

Rais Morsi alitangaza uchaguzi huo awali juma hili, na yeye na chama chake cha Muslim Brotherhood wanatumai hatua hiyo itasaidia kumaliza maandamano ya miezi kadha.
Lakini upinzani unasema hilo ni jaribio jipya la kuhakikisha chama cha Kiislamu kinashikilia madaraka.
