ALIYEKUWA MKUU WA IDARA YA UJASUSI RWANDA, Karegeya aaga dunia mjini Johannesburg



Ramani ya Rwanda

Polisi nchini Afrika Kusini wamesema kuwa aliyekuwa mkuu wa idara ya ujasusi wa Rwanda, Patrick Karegeya, amepatikana ameaga dunia katika hoteli moja mjini Johannesburg.
Bwana Karegeya amekuwa akiishi uhamishoni nchini Afrika Kusini kwa muda wa miaka sita iliyopita.

Karegeya alipokonywa cheo cha kanali baada ya kutofautiana na mshirika wake wa zamani, rais Paul Kagame wa Rwanda, ambaye alimshutumu kwa kuhusika na mashambulio ya kigaidi mjini Kigali.

Katika taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari, na chama cha upinzani cha Rwanda National Congress, RNC, inasema kuwa Karegeya alinyongwa ndani ya chumba chake.

Hata hivyo mamlaka nchini Afrika Kusini haijathibitisha madai hayo.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company