Tanga walalamika maisha magumu

Wazazi na walezi mjini Tanga wamelalamikia hali ngumu ya maisha pamoja na kupanda kwa gharama za vifaa vya wanafunzi shuleni na hivyo, kuitaka Serikali kuwapunguzia kodi wafanyabiashara ili kuweza kumudu gharama za maisha.

Pia wamesema kuwepo kwa kodi nyingi imekuwa chanzo cha maisha kuwa magumu na kuitaka Serikali kuweka afueni katika mambo muhimu ya kijamii ikiwa na pamoja na vifaa vya shule na huduma za kijamii.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakazi hao walisema wafanyabiashara wengi wamekuwa wakiuza bidhaa zao kwa bei ya juu kutokana na kuelemewa na kodi nyingi.
www.hakileo.blogspot.com
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company