Wananchi watakiwa kujiandaa kwa umeme

A umeme official at work Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Mbeya, Crispin Meela amewataka wananchi wa vijiji 35 vya wilaya hiyo ambavyo vipo kwenye mradi wa kupelekewa umeme mapema mwaka huu kuanza kujiandaa kwa kuweka miundombinu iliyo bora kwenye nyumba zao.

Meela alitoa kauli hiyo juzi wakati akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Ibungila Kata ya Malindo kwenye mkutano wa hadhara wakati akiwa kwenye ziara yake ya kikazi.

Alisema Serikali kupitia Mradi wa Wakala wa Umeme Vijijini (Rea), vijiji 35 vimebahatika kuingia kwenye mradi huo ambao utekelezaji wake utaanza Julai mwaka huu.

Pia aliwataka wabuni miradi ya kiuchumi itakayoendana na uwepo wa nishati hiyo.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company