Zitto aungana na CCM kutaka kura ya wazi

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), ameunga mkono msimamo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa kuwataka wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kupiga kura ya wazi katika kufanya uamuzi.

Zitto ameweka wazi msimamo wake jana kwenye kurasa zake za mitandao ya Facebook na Twitter akiwashauri wajumbe wa Bunge hilo kutoendelea na malumbano ya namna ya kupiga kura kati ya zile za siri au za wazi na badala yake kura ya wazi ipewe nafasi.

Alisema: “Nasikia kampeni zinaendelea Dodoma kuhusu uamuzi huo. Siasa zetu tunazifanya ni ‘zero-sum game’, kwamba anayepata anapata vyote, na anayekosa anakosa vyote, haipaswi kuwa hivyo hata kidogo.”

Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company