Edward Moringe Sokoine
Edward Moringe Sokoine (
1938 -
12 Aprili 1984) alikuwa
mwanasiasa kutoka nchi ya
Tanzania.
Aliwahi kuwa
Waziri Mkuu mara mbili, tangu tarehe
13 Februari 1977 hadi
7 Novemba 1980, tena tangu tarehe
24 Februari 1983 hadi
kifo chake, alipofariki kufuatana na
ajali ya gari.
Uongozi wake ulionekana kuwa wa mfano kwa jinsi alivyokuwa na
uadilifu na kufuatilia utendaji kazi huku akikemea ulaji
rushwa na
ubadhirifu wa
mali za umma.
Sokoine alifariki kwa ajali ya gari wakati akitoka kwenye kikao cha
bunge Dodoma kuelekea
Dar es Salaam. Wengi wanashuku ajali hiyo kuwa ilipangwa.
Kifo chake kilileta majonzi makubwa kwa Watanzania wa kawaida ambao walikuwa wanamtarajia kuwatetea wanyonge na kuinua hali ya maisha yao.
Mwili wa Edward Moringe Sokoine ulizikwa nyumbani kwao
Monduli, mkoani
Arusha.
Chuo cha Kilimo na Mifugo Morogoro kilipewa jina la "Chuo cha Kilimo cha Sokoine" ambacho kwa sasa ni
Chuo Kikuu cha Sokoine.