Iran haitabadili balozi wake katika UN


Makamo wa waziri wa mashauri ya nchi za nje wa Iran amesema nchi yake haifikirii kumteua mtu mwengine kuiwakilisha nchi katika Umoja wa Mataifa.

Taarifa iliyotolewa na Abbas Araqchi imesema Iran itatumia sheria kupinga uamuzi wa Marekani wa kumkatalia visa Hamid Abutalebi kuingia Marekani, ili kuwa mwakilishi mpya wa Iran katika Umoja wa Mataifa mjini New York.

Bwana Abutalebi amehusishwa na kundi lilovamia ubalozi wa Marekani mjini Teheran mwaka wa 1979, na nchini Marekani baadhi ya wanasiasa wamepinga vikali uteuzi wa mwanabalozi huyo.

Marekani haikuwahi kumkatalia visa mwakilishi katika Umoja wa Mataifa, wenye makao yake makuu mjini New York.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company