
Juu kwa juu: Cristiano Ronaldo (katikati) akiwa ameruka juu zaidi ya Alaba (wa pili kushoto) na Dante kuwania mpira wa juu katika Nusu Fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya jana Uwanja wa Bernabeu mjini Madrid, Hispania. Real ilishinda 1-0.

Franck Ribery wa Bayern Munich (kushoto) akimfukuzia Daniel Carvajal wa Real

Mfungaji wa bao pekee la Real, Karim Benzema akishangilia baada ya kufunga Uwanja wa Santiago Bernabeu

Kula gwala, kamalizie kazi: Ronaldo akimpisha Gareth Bale dakika ya 74

Philipp Lahm na Gareth Bale (kulia wakigombea mpira wa juu

Beki Mbrazil wa Bayern, Dante (kushoto) akipitia mpira miguuni mwa Angel di Maria wa Real

Thomas Muller (katikati) wa Bayern akililia penalti

Beki wa Real Madrid, Sergio Ramos (kushoto) akiosha mbele ya mshambuliaji wa Bayern, Bastian Schweinsteiger

Schweinsteiger akimdhibiti kiungo wa Real Madrid, Xabi Alonso (katikati)

Mabeki wa Real, Pepe (kushoto) na Sergio Ramos (katikati) wakienda hewani kuondosha hatarini mpira wa juu kutoka kwa Ribery

Kipa wa Real, Iker Casillas (kulia) akiokoa mpira kichwani kwa Javier Martinez

Cristiano Ronaldo akimtoka Jerome Boateng