Watu 683 wahukumiwa kifo nchini Misri

CHANZO BBC SWAHILI

Baadhi ya jamaa wa watuhumiwa waliohukumiwa kifo walizirai baada ya kupokea taarifa

Jaji wa mahakama nchini Misri, amewahukumu kifo watu 683 akiwemo kiongozi wa kundi la Muslim Brotherhood Mohammed Badie.

Mawakili wa watuhumiwa wanasema kuwa wateja wao walikabiliwa na makosa mengi yakiwemo, kushambulia kituo cha polisi mjini Minya mwaka 2013 ambapo polisi mmoja aliuawa.

Jaji huyo pia alibatilisha hukumu ya kifo iliyotolewa kwa watu 492 kati ya watu 529. Hukumu hiyo ilipitishwa mwezi Machi na sasa watahudumia kifungo cha maisha jela.

Kesi na kasi ya kuzisikilizwa kwa kasi hizo, imesababisha hasira na kukosolewa na shirika la kutetea haki za binadamu la Umoja wa Matifa UN.

Kadhalika shirika la Huma Rights Watch limelalamika kuwa kesi hizo zilisikilizwa tu kwa saa chache huku mahakama ikiwazuia mawakili kuwawakilisha washitakiwa.

Duru zinasema kuwa jamaa wa watuhumiwa waliokuwa wanasubiri nje ya mahakama walizirai baada ya kupokea taarifa za hukumu hiyo.

Mwezi jana shirika la kutetea haki za binadamu la Umoja wa Mataifa, lililaani kesi hizo likisema kuwa zinakiuka sheria ya kimataifa ya haki za binadamu.

Msemaji wa shirika hilo, Navi Pillay, alisema kuwa kesi hiyo ilikumbwa na makosa mengi ya utarataibu.

Maafisa wa utawala nchini Misri wamekuwa wakiwasaka na kuwakamata wapiganaji wa kiisilamu na wanachama wa vuguvugu la Muslim Brotherhood ambao walimuingiza mamlakani aliyekuwa Rais Mohammed Morsi ambaye baadaye aliondolewa na Julai.

Mamia wameuawa huku maelfu ya raia wakikamatwa.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company