WAZIRI LUKUVI AZIDI KUANDAMWA


Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu,William Lukuvi.
Jumuiya ya Taasisi za Kiislamu nchini, imemtaka Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, William Lukuvi, (pichani) kujiuzulu wadhifa wake kutokana na kauli yake ya kwamba serikali tatu ikipitishwa jeshi litatwaa madaraka.
Kwa mujibu wa taasisi hiyo, kauli hiyo ya Lukuvi ni kuleta uchochezi.

Lukuvi anadaiwa kuyatoa maneo hayo katika Kanisa la Methodist Jimbo la Dodoma wakati wa sherehe za kumtangaza Mchungaji Joseph Bundala, kuwa Askofu.

Kadhalika, Lukuvi anadaiwa kusema kuwa wanaotaka nchi yao hawawezi kujitegemea bali wanataka serikali ili wapate nafasi ya kujitangaza kuwa nchi ya Kiislamu.

Pia anadaiwa kutamka kwamba Jumuiya ya Uamsho ni taasisi ya Waislamu wenye msimamo mkali.

Kauli ya hizo zilitolewa na Msemaji wa jumuiya hiyo, Rajabu Katimba, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika Msikiti wa Mtambani wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam jana.

''Kauli hizo zinaonyesha Lukuvi ni mmoja wa mawakala wa mfumo kandamizi wa muda mrefu," alisema.

Alisema kuwa Waislamu hawakutarajia waziri mwenye mamlaka makubwa na aliyeaminiwa na Rais na kumwakilisha Waziri Mkuu kutamka kauli za uchochezi tena kanisani.

"Kama alikuwa akisisitiza amani, mbona hakuzungumzia ulipuaji wa mabomu unaoendelea Arusha, tena mpaka kanisani, na je wale ni Uamsho,? Alihoji.

Alisema mpaka sasa uchunguzi wa milipuko ya mabomu Arusha, haijawekwa wazi wala kuwataja wahusika.
                                        CHANZO: NIPASHE
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company