Iran yataka vita dhidi ya Houthi kukoma

Rais Hassa Rouhani wa Iran

Rais wa Iran Hassan Rouhani, ametoa wito wa kusitishwa kwa mashambulio dhidi ya wapiganaji wa Kihouthi nchini Yemen, akiyataja kama makosa makubwa.

Iran pia imepinga madai ya Saudi Arabia kuwa utawala wa Tehran unawapa wapiganaji hao wa Kihouthi ambao ni wa shia mafunzo ya Kijeshi.

Balozi wa Saudi Arabi mjini Tehran, alishutishwa kufika mbele ya wizara ya mambo ya nje ya Iran, kupokea rasmi malalamishi ya Iran.

Nchini Yemen, Ndege za kivita za muungano unaongozwa na Saudi Arabia, zimefanya mashambulio zaidi ya anga dhidi ya wapiganaji wa Houthi katika maeneo ya Kaskazini, Kusini na kati kati mwa Yemen.

Wapiganaji hao wa Houthi ambao wanapinga utawala wa rais Abd Rabbu Mansour Hadi, wamechukua uthibiti wa maeneo kadhaa nchini humo katika miezi ya hivi karibuni.

Akiongea mjini Tehran, rais Rouhani alitaja mashambulio hayo kama makosa makubwa.

Awali waziri wa mambo ya nje wa Marekani John kerry alionya Iran dhidi ya kuwaunga mkono wapiganaji hao wa Houthi.

Kerry aliyasema hayo baada ya Iran kutuma manuwari mbili za kijeshi katika eneo la Guba la Aden.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company