Marekani kuimarisha uhusiano na Cuba

Rais Barack Obama na Waziri Mkuu wa Jamaica, Portia Simpson-Miller katika mkutano wa pamoja huko Kingston, Jamaica.

Rais Barack Obama wa Marekani amesema Alhamisi kwamba atafanya uamuzi karibuni iwapo ataiondoa nchi ya kikomunisti ya Cuba kwenye orodha ya mataifa ambayo Marekani inayaona yanafadhili ugaidi.

Akiwa kwenye ziara nchini Jamaica, Bw Obama amesema kwamba wizara ya mambo ya nje imeangalia kwa kina mwenendo wa Cuba kwenye maswala ya ulimwengu na lililobaki ni pendekezo kutoka kwa washauri wake.

Kwa muda sasa, kiongozi huyo wa Marekani ameashiria kuiondoa Cuba kwenye orodha hiyo, ikiwa mojawapo ya juhudi za kurejesha uhusiano wa kidiplomasia baina ya nchi hizi mbili ambao aliutangaza mwishoni mwa mwaka jana baada ya kuitenga nchi hiyo kwa zaidi ya miongo mitano.

Nchi nyingine tatu ambazo Marekani imeziorodhesha kama wafadhili wa ugaidi ni Syria, Iran na Sudan. Uamuzi huo wa Bw Obama una uwezekano wa kufanyika baadaye wiki hii pale atakapokutana na rais wa Cuba, Raul Castro mjini Panama kuhudhuria kikao cha mataifa ya amerika.
Share this article :
 
Support : Creating Website | SAMBA Template | HAKI LEO Template
Copyright © 2011. HAKI LEO - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by HAKI LEO Template
Imewezeshwa na Haki Leo Company